Waziri
wa Katiba na Sheria Zanzibar Aboubakar Khamis Bakar akizungumza na
wananchi waliohudhuria katika Mkutano wa kujadili Mswaada wa Sheria ya
Upatikanaji wa Katiba Mpya uliofanyika katika Ukumbi wa Baraza la
Wawakilishi la zamani Kikwajuni Mjini Zanzibar.
Rashid
Yussuf Mchenga mmoja ya wachangiaji akitoa maoni yake katika Mkutano wa
Mswaada wa Sheria ya Upatikanaji wa Katiba Mpya uliofanyika katika
Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la zamani Kikwajuni Mjini Zanzibar.
---
FAKI MJAKA NA ZAHIRA BILAL-MAELEZO ZANZIBAR
Waziri
wa Katiba na Sheria Zanzibar Abubar Khamis Bakar amewasihi Wazanzibari
kwa nafasi zao watumie fursa muhimu iliyopo kwa sasa kujadili Mswada wa
Sheria ya Katiba kwa lengo la kupata Katiba Mpya yenye maslahi ya
Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla.
Waziri
huyo ameyasema hayo leo katika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la
zamani Kikwajuni Zanzibar alipokuwa akizungumza na Wananchi,Wanasiasa
pamoja na Waandishi wa Habari kuhusiana na Mswaada wa Utaratibu wa
kupatikana kwa Katiba Mpya.
Amesema
upatikanaji wa Katiba Mpya yenye maslahi kwa Wazanzibari inatokana na
kuwepo kwa umoja na uzalendo ambao unatanguliza maslahi ya Zanzibar
mbele na siyo kujali maslahi ya Vyama.
Abuubakar
amewataka pia wananchi wa Zanzibar kujikusanya na kuipitia Katiba
iliyopo na kuyajadili mapungufu yaliyomo katika katiba hiyo ili muda
utakapofika wa kutoa maoni juu ya Katiba Mpya waweze kufanya hivyo.
Aidha
amesema mswaada huo Mpya ambao umepitishwa karibuni na Bunge la Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania ambao pia unasubiri kutiwa saini na Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni mzuri na wenye kujali maslahi ya
Zanzibar.
Waziri
huyo wa Katiba na Sheria Zanzibar amewatahadharisha wananchi kuwa
makini na watu ambao wanaweza kuwapotosha wananchi katika kipindi hiki
cha kujadili mchakato wa kupata Katiba Mpya.
Amesema
kwamba wananchi wanapaswa kuitumia fursa adhimu waliyoipata kipindi
hiki na kwamba kama hawatoitumia vizuri wanaweza kuijutia katika maisha
yao.
Kwa
upande wa wananchi waliochangia katika mkutano huo wamewaomba viongozi
na wanasiasa kupita katika Majimbo yao ili kuendelea kuwaelimisha
wananchi juu ya upatikanaji wa Katiba Mpya
Aidha
wameviomba vyombo vya Habari Zanzibar kuandaa vipindi mbalimbali na
kushiriki kikamilifu katika Makongamano na Warsha mbali mbali juu ya
Upatikanaji wa Katiba hiyo
Mkutano
huo ambao ulikuwa wa aina yake na kuhudhuriwa pia na baadhi ya Mawaziri
wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wananchi walipata fursa ya kutoa
maoni yao juu ya Mswaada huo.
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)