Vodacom
Miss Tanzania 2011 Salha Israel akifurahia jambo wakati akimkabidhi
fulana Mwenyekiti wa kamati ya Uratibu wa Tamasha la utamaduni wa watu
wa mkoa wa Rukwa na Mkoa tarajiwa wa Katavi Mwangaza Msongole.
Katikati ni Meneja Mawasiliano wa Vodacom Salum Mwalim. Vodacom
imekabidhi fulana elfu moja zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni
kumi na nne kusaidia hamasa ya tamasha hilo.
Meneja
Uhusiano wa Vodacom Tanzania Matina Nkurlu kushoto na Meneja
Mawasiliano wa kampuni hiyo Salum Mwalim wakijadili jambo na Vodacom
Miss Tanzania 2011 Salha Israel wakati wa makabidhiano ya fulana elfu
moja zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni kumi na nne zilizotolewa
na Vodacom Tanzania,kwa ajili ya kufanikisha tamasha la utamaduni wa
watu wa mkoa wa Rukwa na Mkoa tarajiwa wa Katavi litakalofanyika ijumaa
katika kijiji cha makumbusho jijini Dares salaam.
Mwenyekiti
wa kamati ya Uratibu wa Tamasha la utamaduni wa watu wa mkoa wa Rukwa
na Mkoa tarajiwa wa Katavi Mwangaza Msongole kulia akiongea na
waandishi wa habari kuhusiana na tamasha la utamaduni wa watu wa mkoa
wa Rukwa na Mkoa tarajiwa wa katavi litakalofanyika ijumaa katika
kijiji cha makumbusho mara baada ya Vodacom Miss Tanzania 2011 Salha
Israel(katikati) kumkabidhi msaada wa fulana elfu moja zenye thamani ya
zaidi ya shilingi milioni kumi na nne zilizotolewa na Vodacom
Tanzania,kushoto ni Meneja Mawasiliano wa Vodacom Salum Mwalim.
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)