Ndg.Wilfred Lwakatare akitoa maneno ya
kufariji familia ya Mbwana muda mfupi kabla ya kutoa rambirambi
Hapa akimkabidhi fedha bi Hawa
Abdallah,ambaye ni mama mzazi wa marehemu Mbwana Masoud
Mama akilia kwa uchungu baada ya kukumbuka
msiba wa mwanaye baada ya kukabidhiwa fedha za rambirambi
Mzee Yusuph Rule, akiongea kwa niaba ya
familia ya wafiwa.
Chama cha Demokrasia
na Maendeleo mkoa wa kagera, kimetoa shilingi laki tatu na themanini na
nne elfu(384,000/=) kwa familia ya marehemu Masoud Mbwana, mwanachama wa
chama hicho anayedaiwa kuuawa igunga kwenye uchaguzi mdogo wa ubunge
ambapo alikwenda kuwa wakala wa chama chake.Rambi rambi hiyo
imewasilishwa leo Mburahati mtaa wa makurumla kwa Jongo jijini Dar es
salaam,nyumbani kwa marehemu.Aliyewasilisha ubani huo ni ndg W.
Lwakatare mwenyekiti wa mkoa wa Kagera kwa niaba ya viongozi,wanachama
wa Chadema Kagera na wananchi wa mkoa huo.Fedha hizo zimechangwa na
viongozi wa chama hicho waliokuwa na kikao cha kawaida walipopata
taarifa za msiba wa mbwana.Mh.Lwakatare ameomba jamii kuendelea kujali
ndugu wanaofikwa na matatizo.Aliambata pia na katibu mwenezi wa jimbo la
Ubungo ndg Ali Makwilo na katibu wa chama Ubungo ndg Nassoro Balozi.
Picha zimetumwa na Mdau
wa Mjengwablog. aliyeko Dar es salaam.
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)