Taswira Za Misa Ya Miili ya Mapadri Watatu na Kijana Mlei Waliofariki Kutokana na Ajali Ya Gari - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

Taswira Za Misa Ya Miili ya Mapadri Watatu na Kijana Mlei Waliofariki Kutokana na Ajali Ya Gari

Mapadri wakiwa wamebeba moja ya majeneza yenye miili ya mapadri watatu na kijana mlei wakipeleka kwenye gari kwenda kuhifadhiwa vizuri Hospitali ya Agakhan, baada ya kuiombea katika ibada maalumu iliyofanyika jana Kanisa la Katoliki Msimbazi, Dar es Salaam, tayari kusafirishwa nchini kwao Italia kwa mazishi.Walikufa katika ajali ya gari walilokuwa wakisafiria kutoka Kongwa kwenda Dar es Salaam, iliyotokea hivi karibuni eneo la Ruvu, Pwani, baada ya kugongana uso kwa uso na lori.
 
Askofu Mkuu Msaidizi wa Kanisa la Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Salutaris Libena akiiombea miili ya mapadri watatu na kijana mlei katika ibada maalumu iliyofanyika jana Kanisa la Katoliki Msimbazi, Dar es Salaam, tayari kusafirishwa nchini kwao Italia kwa mazishi. Walikufa katika ajali ya gari walilokuwa wakisafiria kutoka Kongwa kwenda Dar es Salaam, iliyotokea hivi karibuni eneo la Ruvu, Pwani, baada ya kugongana uso kwa uso na lori.
Baadhi ya waumini wakilia wakati majeneza yenye miili ya mapadri na Mlei mmoja ikipakiwa kwenye magari baada ya kuombewa.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages