Tanzania yashiriki vyema kwenye Maonesho ya Utalii yaliyofanyika nchini Ungereza (World Travel Market) kuanzia tarehe 7-10 November 2011) - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

Tanzania yashiriki vyema kwenye Maonesho ya Utalii yaliyofanyika nchini Ungereza (World Travel Market) kuanzia tarehe 7-10 November 2011)

Bodi Utalii Tanzania (TTB) ikishirikiana na kampuni mbalimbali za Utalii imeshiriki maonesho ya Utalii yaliofanyika nchini Uingereza yajulikanayo kama World Travel Market kuanzia tarehe 7-10, 2011. Jumla ya kampuni 62 kutoka Tanzania bara na visiwani walishirikia maonesho haya na Waziri wa Maliasili ya Utalii Mheshimiwa Ezekiel Maige na Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Mheshimiwa Abdillah Jihad Hassan viongozi wa wa serikali waliohudhuria maonesho haya. Katika maonesho haya Banda la Tanzania lilikuwa kati ya mabada makubwa kwa upande wa Afrika na lilikuwa na picha zinazoonesha vivutio vya Utalii vya Tanzania vilevile kulikuwepo bango kubwa linalohasisha Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania. Banda la Tanzania lilivyooneka wakati wa maonesho yaliofanyika nchini Uingereza tarehe 7-10 Nov 2011.
Banda la Tanzania lilitembelewa na watu mashuhuri, mmoja wa watu mashuhuri waliotembele banda la TTB ni Mchezaji wa Timu ya Taifa ya Ghana na Timu na anayechezea soka lake katika timu ya Al Ain ya Falme za kiarabu (UAE) i Asamoah Gyan. Asamoh akiwa na baadhi ya raia kutoka Rwanda na pamoja na mmoja wa maafisa wa Bodi ya Utalii Mr Geofrey Meena kwenye maonesho haya yaliofanyika Uingreza Mmoja wa washiriki waliohudhuria maonesho haya alikuwa Mkurungezi Mkuu wa Cordial Tours and Travel Mr David Kizito hapa Mzee Kizito alikuwa katika harakati za kuuza Safari za kuja Tanzania.
Wafanya biashara kutoka Tanzania wakiwajibika kuunza safari za kuja Tanzania (Tour Package)

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages