Naibu Waziri wa
Viwanda na Biashara Mhe. Lazaro Nyarandu (MB) akikata utepe kama ishara
ya kufungua rasmi maonyesho ya 9 ya SIDO ya nyanda za juu kusini
inayoshirikisha mikoa ya Rukwa, Iringa na Mbeya. Kulia kwake
anayeshuhudia ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Joyce Mgana.
Maonyesho hayo yanafanyika katika Uwanja wa Nelson Mandela Mkoani Rukwa
kwa kushirikisha wajasiriamali kutoka zaidi ya mikoa 14 nchini na
wengine kutoka nchi jirani za Kenya na Burundi.
Mkurugenzi
Mkuu wa SIDO nchini Ndugu Mike Laizer akifafanua jambo kwa Naibu wa
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Lazaro Nyarandu kwenye banda la
SIDO. Kulia kwa Naibu Waziri ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Joyce
Mgana.
Uhifadhi
wa Mazingira nao umepewa kipaumbele Mkoani Rukwa, Mjasiriamali wa
uhifadhi wa Mazingira wa kikundi cha REYO akinadi miti aina mbalimbali
inayofaa kwa uhifadhi wa mazingira na matumizi mengineyo katika
maonesho hayo.
Mjasiriamali
wa Rukwa anayejishughulisha na utengenezaji wa viatu kwa kutumia ngozi
mbalimbali. Chipawas Leather Tunning wanapatikana maeneo ya Jangwani
Wilayani Sumbawanga, wapo pia kwenye maonesho hayo.
Haya
mambo ya ajabu pia yapo, inadaiwa ni Mtu wa ajabu kutoka Burundi
aliyezaliwa kichwa kitupu, ana uwezo wa kuzungumza lugha tofauti na
wakati wa kumuhoji alidai kuwa chakula chake ni Sindano maalum. Katika
akili ya kawaida haifikiriki na wengi wa watu waliomtembelea huyu bwana
ikiwa ni pamoja na mimi walisema haya ni MAZINGAUBWE. Huyu bwana
anapatikana kwenye banda moja na ili kuweza kumuona inatakiwa kulipia
shillingi mia tano tu. Nilishuhudia baadhi ya watoto waliopata bahati
ya kumuona wakilia kwa hofu na wengine wakiwa na mshangao mkubwa.
Naibu Waziri akisaini Kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Sumbawanga. Kwa habari zaidi nenda hapa: (http://rukwareview.blogspot.com/)
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)