Mbunge
wa jimbo la Arusha mjini,Godbless Lema,akiwa juu ya gari lake nje ya
uwanja wa Mahakama Kuu kanda ya Arusha,baada ya kupata dhamana katika
kesi ya kufanya maandamano na kufanya mkusanyiko bila kibali cha polisi.
Picha na Filbert Rweyemamu
--
SHUGHULI
mbalimbali za kibiashara na kijamii katika Jiji la Arusha jana
zilisimama kwa muda kupisha mapokezi ya Mbunge wa Arusha Mjini
(Chadema), Godbless Lema baada ya kutoka rumande katika Gereza la
Kisongo alilokaa kwa siku 14.Oktoba 31, mwaka huu, Lema na wenzake 18
walifikishwa mahakamani wakidaiwa kufanya kusanyiko lisilo halali na
kukaidi amri ya polisi iliyowataka watawanyike yeye na
wenzake.Walikamatwa na kufikishwa mahakamani na kudhaminiwa lakini Lema
akikataa dhamana akisema ameamua kutangulia gerezani kudhihirisha kwamba
haogopi gereza.Lema alitoka kwa dhamana na kuandaliwa mapokezi makubwa
ya wafuasi wa Chadema ambayo yaligeuka kuwa maandamano ya
amani.Shamrashamra za mapokezi hayo zilisababisha kusimama kwa muda kwa
shughuli kadhaa kama huduma za kibenki hasa zile zilizo katika Barabara
ya Sokoine.
Wakati wa maandamano hayo wafuasi hao wa Chadema walikuwa wakipeperusha majani na matawi ya miti.
Mahakimu, mawakili na makarani wa mahakama nao walilazimika kuacha shughuli zao kwa muda na kutoka nje kushuhudia mapokezi ya mbunge huyo yaliyokuwa yakipambwa kwa nyimbo mbalimbali nje ya mahakama hiyo.
Sehemu ya nyimbo hizo zilimgusa Mkuu wa Polisi Wilaya hiyo ya Arusha, Zuberi Mwombeji ambaye hivi karibuni aliingia kwenye mvutano mkubwa na chama hicho cha upinzani akituhumiwa kutumia nguvu kuwadhibiti viongozi wake.Waliimba: “Tunamtaka….panya wetu… tunamtaka mbunge wetu… Zuberi (OCD), aondoke. Mlituvizia usiku, leo sasa ni mchana hapatatosha. Hatuandamani, tunampokea shujaa wetu.”
Wakati wa maandamano hayo wafuasi hao wa Chadema walikuwa wakipeperusha majani na matawi ya miti.
Mahakimu, mawakili na makarani wa mahakama nao walilazimika kuacha shughuli zao kwa muda na kutoka nje kushuhudia mapokezi ya mbunge huyo yaliyokuwa yakipambwa kwa nyimbo mbalimbali nje ya mahakama hiyo.
Sehemu ya nyimbo hizo zilimgusa Mkuu wa Polisi Wilaya hiyo ya Arusha, Zuberi Mwombeji ambaye hivi karibuni aliingia kwenye mvutano mkubwa na chama hicho cha upinzani akituhumiwa kutumia nguvu kuwadhibiti viongozi wake.Waliimba: “Tunamtaka….panya wetu… tunamtaka mbunge wetu… Zuberi (OCD), aondoke. Mlituvizia usiku, leo sasa ni mchana hapatatosha. Hatuandamani, tunampokea shujaa wetu.”
Shamrashamra
hizo pia ziliambatana na mabango mbalimbali huku pia kukiwa na fulana
maalumu zilizokuwa zimevaliwa na baadhi ya mashabiki zikiwa na maneno
yaliyosomeka: “Lema kaonyesha njia mbadala ya kudai haki. Jela ni mahali
pa kuishi kama sababu ya kwenda huko ni vitadhidi uonevu, ukandamizaji
wa haki na utu wa binadamu.”
Siasa za nchi hii zinaongozwa na JESHI LA POLISI AU ???????? kitendo alichofanyiwa Lema kina maslahi kwa nani hasa ????????
ReplyDeleteKwa hali hii itafika mahali bungeni, Wabunge pinzani watashindwa Kupeana Salamu