Mke
wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Mama Asha Bilal, akisoma
Hotuba yake wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwa
Taasisi ya Alliance Francaise Jijini Dar es Salaam Tanzania, iliyofanyika jana
usiku kwenye Ukumbi wa Alliance Francaise Dar es Salaam. Katikati ni Balozi wa
Ufaransa nchini, Marcel Escure (kushoto) ni Mkurugenzi wa Taasisi hiyo, Julia
Giannetti.
Mke
wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal,
akizungumza jambo na Mwenyekiti wa Kikundi cha wake wa Mabalozi wa Nchi za
Afrika, Mama Juma Khalfan Mpango, wakati alipokuwa mgeni rasmi katika sherehe za
maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwa Taasisi ya Alliance Francaise
Jijini Dar es Salaam Tanzania, iliyofanyika jana usiku kwenye Ukumbi wa Alliance
Francaise Dar es Salaam. Kushoto ni Rahma Othman.
Mkurugenzi
wa Taasisi hiyo, Julia Giannetti, akizungumza wakati wa sherehe hizo jana
usiku.
Balozi
wa Ufaransa nchini, Marcel Escure, akizungumza wakati wa hafla ya sherehe
hizo.
Baadhi
ya wadau wa Lugha ya Kifaransa waliohudhuria hafla hiyo, wakimsikiliza Mgeni
rasmi Mama Asha Bilal, wakati akitoa Hotuba yake kwa Lugha ya
Kifaransa.
Mke
wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Mama Asha Bilal,
akionyeshwa baadhi ya picha zilizowekwa katika ukumbi huo kwa ajili ya maonyesho
ya maadhimisho hayo.
Kitanda
kilichowekwa kwa ajili ya maonyesho katika Ukumbi huo kikiwa na hostoria ya
pekee, ambapo shuka iliyotandikwa katika kitanda hicho imetengenezwa na
Mwanadada kwa kutumia Bahasha za barua alizokuwa akiandikiwa na kutumiwa na
Marafiki zake wa kiume tangu barua ya kwanza hadi ya mwisho wakati wa usichana
wake wakati akiwa katika nchi mbalimbali duniani na kati ya hao ni wanaume 17
aliweza kutembea nao ambao nao pia amewaandika katika moja ya ua lake
alilolifuma kwa mtindo wa kitambaa chini hapa.
Idadi
ya wanaume aliopata kutembea nao mwanadada huyo kama
alivyowaorodhesha.
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)