Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akisoma hotuba yake wakati akifungua Mdahalo wa Nafasi ya Umuhimu wa
Katiba katika Maisha ya Watanzania, uliofunguliwa leo, katika Jumba la
Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akiongozana na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu
Nyerere, Salim Ahmed Salim (wa pili kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa
Taasisi hiyo, Joseph Butiku (wa pili kushoto) wakati akiiwasili kwenye
Jumba la Makumbusho ya Taifa leo kwa ajili ya kufungua Mdahalo wa Nafasi
ya Umuhimu wa Katiba katika Maisha ya Watanzania.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akitembelea katika maonyesho ya Jumba la Makumbusho ya Taifa kuangalia
picha za baadhi ya Mashujaa wa Harakati za ukombozi zilizowekwa katika
jumba hilo. Katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Taasisi ya
Mwalimu Nyerere, Salim Ahmed Salim na (kulia) ni Mkurugenzi wa Taasisi
hiyo, Joseph Butiku.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akisoma moja ya kitabu kilochokuwa katika meza ya maonyesho ya vitabu
katika Jumba la Makumbusho ya Taifa, baada ya kufungua rasmi Mdahalo wa
wa Nafasi ya Umuhimu wa Katiba katika Maisha ya Watanzania,
uliofunguliwa leo.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wageni waalikwa katika
mdahalo huo kutoka Unguja.
Mwenyekiti
wa Bodi ya Wakurugenzi wa Taasisi wa Mwalimu Nyerere, Salim Ahmed Salim
(kushoto) na Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Sinde Warioba (katikati)
wakiteta jambo na Katibu Mkuu wa Chama cha CHADEMA) Willbroad Slaa, nje
ya ukumbi, wakati Mdahalo wa Nafasi ya Umuhimu wa Katiba katika Maisha
ya Watanzania, uliofunguliwa leo, na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, katika Jumba la
Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)