Moja
ya Transifoma iliyopo katika Kituo cha Umeme cha Ubungo jijini Dar es
Salaam (Ubungo Grid Sub Station) imeungua moto jioni ya jana. Akizungumza
na waandishi wa habari katika eneo la tukio, Naibu Mkurugenzi wa
Tanesco, Bi. Sophia Mgonja amesema kuwa, kutokana na hitilafu hiyo Jiji
la Dar es Salaam na Visiwa vya Zanzibar vitakosa umeme kwa siku kadhaa.
Akifafanua zaidi juu ya tukio hilo, Mgonja alisema lilitokea baada ya
kifaa cha kurekebisha nguvu ya umeme kiitwacho Reactor kuungua. Picha
hizi zinawanyonyesha wafanyakazi wa kikosi cha zima moto wakizima moto
katika Transifoma iliyokuwa ikiungua.
Picha kwa hisani ya Kulwa Mwaibale/Global Publishers .
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)