Mbunge
wa jimbo la arusha mjini Bw. Goodbless Lema leo ameachiliwa huru na
mahakama ya hakimu mkazi mara baada ya kukidhi vigezo vya mahakama
katika kesi ambayo inamkabili mbunge huyo ya kufanya maandamano na
mkusanyiko bila kibali maalumu cha vyombo vya usalama.
Hayo yalikuja mara baada kudaiwa
mahakamani hapo kuwa mtuhumiwa namba moja ambaye ni Mbunge wa jimbo la
arusha mjini kuwa nje kwa dhamana hadi Disemba 14 mwaka huu
Aidha hakimu ambaye anasikiliza
kesi hiyo Bi Judith Kamala aliiambia mahakama kuwa mtuhumiwa huyo
kisheria yupo huru kwa kuwa vigezo vya mahakama vilidai kuwa mtuhumiwa
huyo namba moja anatakiwa kuwa na wadhamini wawili jambo ambalo
walikidhi vigezo
hata hivyo kesi hiyo iliahirishwa ambapo itasikilizwa tena mahakamani hapo Disemba 14 mwaka huu.
Katika hatua nyingine mbunge huyo aliambia vyombo vya habari kuwa
mkuu wa Mkoa wa Arusha Bw Magesa
Mulongo anatakiwa kuacha ushabiki wa kisiasa na kama hataweza kuacha
ushabiki huo atalazimika kuwatumia wanawake yaani mke wa mbunge na mke
wa mkuu wa mkoa ili waweze kusuluishana.
Aidha Bw. Lema alisema kuwa hatua
hiyo itakuja kwa kuwa mara nyingi mkuu huyo ameonekana akisema na
kuwatetea chama cha mapinduzi hali ambayo inachangia unyanyasaji mkubwa
sana
Aliongeza kuwa hali hiyo ya
kumtuma mke wake kwenda kwa RC mkoa wa Arusha huenda ikaleta maafanikio
zaidi kwa kuwa wanawake kwa wanawake wanaweza kusikilizana tofauti na
wao ambao mpaka sasa tofauti zimeshajitokeza sana.
katika hatua nyingine Bw Lema
aliongeza kuwa wananchi wanapaswa kujua na kutambau kuwa yeye si mwehu
kukataa dhamana na badala yake wanatakiwa kujua kuwa anatafuta haki
ambayo inaondolewa na baadhi ya vyama vya siasa pamoja na Jeshi la
polisi
Alibainisha kuwa kwa kuwepo kwake
Gerezani ameweza kugundua na kujua kuwa ndani ya jeshi la polisi wapo
baadhi ya askari ambao wanakiuka taratibu za jeshi hilo na kuwapa watu
kesi ambazo si za kwao hali ambayo inasabbaisha madhara makubwa sana
kwa wananchi hasa wale wenye kipato cha chinil.
Bw Lema alisema kuwa wananchi
wanatakiwa kuhakikisha kuwa wana kemea vibaya tabia ya kunyimwa haki zao
za msingi na pia wananchi hao wana haki
-
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)