Watu
zaidi ya 35 wamejeruhiwa katika ajali yak basi iliyotokea maeneo ya
Kongowe mkoani Pwani. Mashuhuda wamelitaja basi hilo kuwa ni DELUX
coach, ambalo lililokuwa linatoka Dar es salaam, kuelekea mkoani Dodoma,
mchana wa jana , ambapo lilipinduka na kuungua huku ndani likiwa na abiria
na hivyo kuzusha hofu kwa ndugu na jamaa ambao wamesafirisha jamaa zao
katika gari hilo.
Afisa habari hospitali ya Tumbi mkoani Pwani, Bi rose Mtei anaweka wazi idadi hiyo ya majeruhi waliopokelewa hospitalini hapo na hali za majeruhi.
Hata hivyo ofisa uhusiano huyo, alikiri kutopokelewa kwa maiti yoyote katika hospitali hiyo, na jitihada za kutafuta kamanda wa polisi mkoa ili kuzungumzia hilo hazikufanikiwa baada yak simu yake kuita bila mafanikio.





No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)