Maafisa Waandamizi Wa Ofisi Za Balozi Za Tanzania Wapigwa Msasa - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

Maafisa Waandamizi Wa Ofisi Za Balozi Za Tanzania Wapigwa Msasa

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa John Haule akifungua mafunzo ya wiki tatu ya kuwajengea uwezo wa kazi maafisa waandamizi wa ofisi za balozi za Tanzania na maafisa wa wizara hiyo yaliyoandaliwa na chuo cha Diplomasia kilichopo Kurasini jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya wiki tatu ya kuwajengea uwezo wa kazi maafisa wa Serikali yaliyoandaliwa na Chuo cha Diplomasia kilichopo Kurasini jijini Dar es Salaam wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa John Haule (hayupo pichani) wakati akifungua mafunzo hayo. Washiriki wa mafunzo hayo ni maafisa waandamizi wa ofisi za balozi za Tanzania na maafisa wa wizara hiyo.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya wiki tatu ya kuwajengea uwezo wa kazi maafisa wa Serikali yaliyoandaliwa na Chuo cha Diplomasia
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa John Haule akiongea jambo na Balozi Dk. Mohammed Maundi (kushoto) ambaye ni Mkuu wa Chuo cha Diplomasia (kushoto) na Mwenyekiti wa bodi ya chuo hicho Balozi Charles Sanga (kulia) mara baada ya kumalizika kwa ufunguzi wa mafunzo ya wiki tatu ya kuwajengea uwezo wa kazi maafisa waandamizi wa ofisi za balozi za Tanzania na maafisa wa wizara hiyo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa John Haule (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na maafisa waandamizi wa ofisi za balozi za Tanzania na maafisa wa wizara hiyo ambao ni washiriki wa mafunzo ya wiki tatu ya kuwajengea uwezo wa kazi yaliyoandaliwa na Chuo cha Diplomasia kilichopo Kurasini jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages