
Jeshi
la Polisi nchini (PT) kupitia Inspekta Generali wake Said
Mwema(Pichani) imetangaza dau la Shilingi Milioni 5 kwa mtu yeyote
atakaefanikisha kupatikana kwa mtu aliyemjeruhi mtoto Adam Robert (14)
ambaye ni Albino huko Geita ambapo mtu asiyejulikana alimvamia mtoto
huyo na kuanza kumkata kata mikono na kisha kutoweka na vidole vya
Albino huyo.
Tukio
hilo lilitokea usiku wa kuamkia mwishoni mwawiki katika Kijiji cha
Nyaruguguna, Kata na Tarafa ya Nyang’hwale ambapo mlemavu huyo, Adam
Robert (14), mwanafunzi wa darasa la nne, alivamiwa na kukatwa mkono wa
kulia na kisha kunyofolewa vidole vitatu vya mkono wa kushoto.





No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)