Benki ya NBC yazindua Wiki ya Huduma kwa Wateja - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

Benki ya NBC yazindua Wiki ya Huduma kwa Wateja

Meneja Huduma kwa Wateja wa Benki ya NBC, Jane Dogani (katikati) akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa Wiki ya Huduma Kwa Wateja wa benki hiyo jiijini Dar ers Salaam jana. Kushoto
ni Allan Maro na Mark Peter maofisa wa NBC katika kitengo cha Huduma kwa Wateja.
 
NATIONAL BANK OF COMMERCE
                                TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
            BENKI YA NBC YAZINDUA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA
Dar es Salaam Oktoba 17, 2011
BENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua Wiki ya Huduma kwa Wateja inayoanza leo hadi tarehe 22 Oktoba mwaka huu. NBC inaadhimisha Wiki ya Huduma kwa Wateja inayoanza leo  katika matawi yote ya benki hiyo nchini ikiwa na kauli mbiu ya ‘Mteja Kwanza’

Akizungumza Meneja wa Kitengo cha Huduma Bora kwa Wateja wa Benki ya NBC, Mama Jane Dogani anasema kauli mbiu ya Wiki ya Huduma kwa Wateja ya NBC inayosema  ‘Mteja Kwanza’ ni dhihirisho la jinsi gani mteja wa benki hiyo alivyo muhimu na kuwa mhimili mkuu wa maendeleo ya Benki ya NBC.
“Madhumuni makubwa katika wiki hii ni kutaka kuwa karibu zaidi na wateja wetu ili tuweze kubadilishana mawazo tupokee maoni yao kuhusu ni nini wangependa tuwafanyie au ni wapi na kipi wangependa tukibadilishe ama kukiongeza,” anasema Mama Dogani.

Katika Wiki hii ya Huduma kwa Wateja wa NBC wateja wanaweza kufika katika matawi ya benki hiyo, kuuliza maswali kuhusu huduma na bidhaa  mbalimbali zinazotolewa na NBC. “Wataalamu wetu wamejipanga vizuri katika matawi yote ya benki yetu hivyo wateja msisite kufika katika matawi hayo ambako mtapata majibu sahihi kuhusu huduma zetu, aina mbalimbali ya akaunti tunazotoa, bidhaa na huduma mpya, masuala ya mikopo na mambo yoyote ya kibenki yanayoihusu NBC,” anasema. 

Katika Wiki ya Huduma kwa Wateja NBC mbali na kuandaa mikutano na wateja wake watakaofika katika matawi hayo pia imeandaa  zawadi mbalimbali kwa baadhi ya wateja wake ikiwa kama ishara ya shukurani kwa wateja wake na pia kufurahia mafanikio ya benki yao iliyo karibu kila mahali yaani Benki ya NBC.
“Itakuwa wiki yenye mambo mengi ya kuvutia kutoka NBC, natoa wito kwa wateja wetu wasikose kutembelea matawi yetu kujionea wenyewe jinsi benki yao ilivyojipanga kuwahudumia.Wale ambao hawajafungua akaunti nasi basi huu ndio wakati muafaka wa kufika katika matawi yetu kufungua akaunti na kupata huduma za kibenki kutoka kwa wahudumu wetu wapole na wakarimu,” anasema Mama Dogani.

Benki ya NBC iliundwa Aprili 1, 2000 baada ya ubinafsishwaji na kuuzwa kwa Benki ya ABSA ya Afrika Kusini inayomiliki Hisa asilimia 55  huku Serikali ya Tanzania ikibaki na Hisa za asilimia 30 na zinazobaki asilimia 15 zikimilikiwa na Mashirika ya Kimataifa ya Kifedha.  Benki ya NBC ina mtandao wa matawi 53 nchini kote na mashine za kutolea fedha (ATM) zaidi ya 250.
MWISHO.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages