WAZIRI SOFIA SIMBA AZINDUA MAONYESHO YA TWENDE VIWANJA VYA MNAZI MMOJA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

WAZIRI SOFIA SIMBA AZINDUA MAONYESHO YA TWENDE VIWANJA VYA MNAZI MMOJA

Waziri wa maendeleo ya jamii, jinsia na watoto, Sofia Simba akizungumza na mmoja ya wanawake Wajasirilamali waliojitokeza kushiriki maonyesho ya wajasiriamali wanawake yaliyoandaliwa na mbunifu maarufu wa mavazi na mitindo Mustafa Hassanali kwenye viwanja vya Mnazi mmoja jijini DAr es Salaam.
Kwa wenye watoto ambao mnataka wavae mavazi ya kisasa dada Husna anawakaribisha ZERO 2 TWELVE BABY SUPER STORE, lililolopo Tranic Plaza, Ada Estate.
Asali, asali asali kutoka kwetu TABORA, kuna asali ya nyuki wadogo na wakubwa.Kama mjuavyo asali inatumika kutibu magonjwa mengi ya binadamu hivyo ni muhimu kutembelea hapo na kupata mafunzo ya matumizi ya asali kama tiba ya magonjwa mbalimbali.
FEMINA  hip nao wapo
Hapa Waziri Simba akipata amaelezo toka kwa mmoja ya washiriki katrika maonyesho hayo akiwakilisha Taasisi ya Maisha Bora, hwa wapo msasani mwisho wakijihusisha na masuala ya afya ambapo wana kifaa maalum cha kumuwezesha mtu kujua magonjwa yanayomkabili mtu, pia wanatoa sumu mwili n.k,
Product za LUMULI hizi ni sabuni za maji mahususi kwa kusafishia choo, kufulia na hata kuonshea vyombo
Shea Butter hii ni bidhaa inayotengenezwa kwa mchanganyiko wa aina mbalimbali za mafuta ya asili yenye tiba mbalimbali za ngozi, wana mafuta ambayo yanaifanya ngozi iwe nzuri na ya kuvutia, mafuta ya kurutubisha nywele, yanayosaidia kuondoa makunyanzi, kuondoa michiriki, chunusi, maumivu ya misuli n.k, waweza tembelea http://www.tausisheabutter.com/ ili upate mambo zaidi.Picha Zote Kwa Hisani Ya Dina Ismail - Mamapipiro Blogu

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages