WAWAKILISHI WA TANZANIA KATIKA BUNGE LA VIAJANA NCHINI LONDON - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

WAWAKILISHI WA TANZANIA KATIKA BUNGE LA VIAJANA NCHINI LONDON

Wawakilishi wa vijana wa Tanzania katika Bunge la Vijana wakipozi kwa picha katika Ofisi za Ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza baada ya kuwasili nchini humo kwa ajili ya kuwakilisha vijana katika Bunge hilo.
Ubalozi wa Tanzania Nchini Uingereza Kwa Kushirikiana na Ofisi ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa  Tanzania wamewateua Linda Kapinga na Lucy Minde kutuwakilisha katika mkutano wa nne wa Commonwealth Youth Parliament ( Bunge la Vijana) ulioanza tarehe 6-10 Septemba 2011 jijini London. 

Wawakilishi hao wakiwa katika mahojiano.
Mkutano huo Umeandaliwa na Commonwealth Parliamentary Association tawi la Uingereza ikishirikishwa na Sekretarieti ya CPA ambayo ni Umoja wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola. Katibu wake ni Mwafrika wa kwanza kuteuliwa na Pia ni Mtanzania mwenzetu Dr William Shija.
Pozi la picha Ubalozini hapo.  
Lengo kuu la mkutano huu ni kuwawezesha vijana kati ya miaka 19-29 kwa kuwapatia uzoefu wa shughuli za Bunge hasa katika kuimarisha demokrasia ya mabunge na Uchumi. Motto wa Mkutano wa mwaka huu "MABADILIKO YA HALI YA HEWA"

Ubalozi wa Tanzania hapa Uingereza unapenda kuwapongeza sana Linda Kapinga na Lucy Minde kwa kuchaguliwa kwao na pia kuwatakia kila la kheri katika kutuwakilisha kwenye mkutano huu.
Mahojiano yanaendelea.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages