Wanaharakati waongelea siku ya haki ya kupata taarifa - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

Wanaharakati waongelea siku ya haki ya kupata taarifa

Dr Sengondo Mvungi kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam akichangia mada ya umuhimu wa sheria ya habari na haki ya mtanzania kupata, kupewa na kutafuta habari.Mjadala huu ulirushwa moja kwa moja na kituo cha redio cha Wapo FM, ambapo matangazo yalirushwa kutokea ofisi za HakiElimu.

Mdahalo huo umefanyika leo ikiwa ni kilele cha maadhimisho ya wiki ya haki ya kupata taarifa duniani.Tangu mwaka 2007, wadau wa habari na watanzania kwa ujumla wamekua wakidai kuwepo kwa sheria ya habari (Right to information law), lakini hadi sasa imekua kitendawili.

Mwandishi na mtangazaji wa kituo cha redio cha Wapo FM akiongoza mjadala huo
Mafundi mitambo nao walikuwepo kuhakikisha matangazo yanaruka bila mtafaruku wowote
Picha Zote Na Haki Elimu

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages