Vodacom Tanzania Yadhamini Mbio Za Mashua Za Tanzacat - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

Vodacom Tanzania Yadhamini Mbio Za Mashua Za Tanzacat


Baadhi ya Washiriki wa Mbio za Mashua, zijulikanazo kama TANZACAT wakipunga Mikono kuashirika  kuanza kwa  mbio  hizo zilizozinduliwa rasmi jana katika Klabu ya Yatch jijini na kudhaminiwa na kampuni ya Simu za Mkononi ya Vodacom Tanzania. 
Baadhi ya Washiriki wa Mbio za Mashua, Zijulikanazo kama TANZACAT wakianza Mbio hizo jana katika Ufukwe wa bahari ya Hindi eneo la Klabu ya Yatch  jijini Dar es Salaam ambapo Mashindano hayo yanayochukua siku saba yanadhaminiwa na kampuni ya Simu za Mkononi ya Vodacom Tanzania.
Mwenyekiti wa mbio za mashua Nicholus Zervos akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mbio hizo zilizoshirikisha mataifa 16 na kuwashukuru wadhamini wakuu Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania. 
Mshiriki wa Mbio za Mashua zijulikanazo kama TANZACAT, Belia Klaassen, aliyewahi kushiriki mbio hizo kwa  miaka kumi nchini Tanzania  akielezea namna anavyofurahia kushiriki mashindano hayo tena  na jinsi yalivyoboreshwa zaidi jana jijini Dar es salaam
Mmoja wa washiriki wa mbio za mashua zijulikanazo kama TANZANCAT Evelyne Geubbels (kulia) akieleza namna mbio hizo za ufunguzi zinazodhaminiwa na Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania zilivyofana katika Klabu ya Yatch jijini, kushoto ni mshiriki mwenzake Jerome Vant Pad Bosch.
Mwenyekiti wa mbio za mashua Nicholus Zervos (wa pili kulia)akiwa na baadhi ya washiriki wa mbio hizo mara baada ya ufunguzi wa mbio hizo jana jijini ambapo zitaendelea kwa muda wa siku saba na kudhaminiwa na kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages