URBAN PULSE NDANI YA SPORAH SHOW!! - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

URBAN PULSE NDANI YA SPORAH SHOW!!

Frank akijadiliana na Mish wakati wa kipindi cha chemsha Bongo


                                                      Mish akikamua ndani ya Sporah show   
Urban pulse Ndani ya sporah show
Kwa mara nyingine tena Frank toka Urban pulse na msaniii makini Fyah Sister wakiwa ndani katika studio za Televisheni zinazotengeneza kipindi mashuhuri cha Sporah Show.
 
Kipindi hiki  maarufu kiendeshwacho na Dada yetu Sporah hapa UK kinapatiakana katika Sky TV  chaneli 184. Frank na Fyah Sister walialikwa kwenye exclusive interview na Dada Sporah kuzungumzia hali ya promotion ya nyimbo na mixtape ya fyah sister iliyopo mtaani hivi sasa. Vilevile walizungumzia hali ya uhusiano wa ma promoter na wasanii pamoja  na mitihani gani wanakumbana nayo.
 
 Album ya Fyah Sister ambayo imetengenezwa katoka studio za urban pulse, ni moja ya albamu zinazokuja juu sasa hasa katika kundi la wasanii wa kike, kwani England kuna wasanii wachache sana wazuri wa kike. Pia kipindi kiliongelea hatua na mafanikio ambayo urban pulse wameyapata mpaka hivi sasa kwenye masuala ya mbalimbali. Unaweza kudownload au kusikiliza mixtape ya Mish inayoitwa Fire Brigade kupitia link hapo chini

http://www.datpiff.com/Mish-Da-Fyah-Sis-Fyah-Brigade-mixtape.238903.html
Mish ni msanii mkali wa kike anaekuja juu hapa UK, amefanya maonyesho mengi ikiwepo Notting Hill Carnival, Derby, Centre Hall Westminister jijini london n.k. Pia amechaguliwa kuingia katika mchakato wa kumtafuta best MC katika shindano linaloitwa OPEN MIC litakalofanyika mwezi wa kumi na fainali zake kufanyika katika O2 Arena london.

Spora show imekuwepeo mstari wa mbele katika kusaidia, kuwahamisha  wafanyabiashara na wanaharakati wa Kiafrika hapa UK. Vilevile ni kipindi kinachopigania na kuangaza mapambano kuhusu maswala yanayowakabili jamii za kiafrika  uk, kama vile, domestic violence,child abuse,rape, teenage pregnancy na masuala mengine yanayoathiri jamii zetu.

Kipindi Hiki kitakuwa hewani mda sio mrefu kupitia Ben TV sky channel 184. Kwa maelezo zaidi tembelea Sporah Show Blog

Asanteni,

URBAN PULSE CREATIVE

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages