TIMU YA MADAKTARI WA MACHO WATOA HUDUMA YA UPASUAJI WA MTOTO WA JICHO MKOANI SINGIDA KWA MSAADA WA MBUNGE DEWJI. - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

TIMU YA MADAKTARI WA MACHO WATOA HUDUMA YA UPASUAJI WA MTOTO WA JICHO MKOANI SINGIDA KWA MSAADA WA MBUNGE DEWJI.

: Dk. Padhani akiwa kazini akimfanyia upasuaji wa macho mmoja wa wagonjwa wa macho 100 wanaotarajiwa kufanyiwa upasuaji.
Baadhi ya wagonjwa wa macho wakiwa kwenye dirisha la mapokezi la hospitali ya mkoa iliyopo mjini humo kwa ajili ya kujiandakisha.
Baadhi wa waginjwa wa macho wanaosubiri kufanyiwa upasuaji.
Na.Nathaniel Limu
Wagonjwa wa macho zaidi ya mia moja (100) kutoka sehemu mbalimbali za mkoa wa Singida,wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji mbalimbali ukiwemo wa kutoa mtoto wa jicho, katika kipindi cha siku tatu mfululizo kuanzia jana (16/9/2011).
Wagonjwa hao ambao wanafanyiwa upasuaji na kupewa huduma ya malazi bure, zoezi hilo linaendelea kufanyika katika wodi ya macho iliyopo katika hospitali ya mkoa mjini Singida.
.
Akizungumza na waandishi wa habari jana,kiongozi wa timu ya madaktari inayosimamia zoezi hilo, Dk.Dh.Padhani, amesema zoezi hilo linafanywa kwa ushirikiano wa pamoja na madaktari wa macho kutoka hospitali ya taifa ya Muhimbili na shirika lisilo la kiserikali la Bilali Muslim Mission la jijini Dar-es-salaam.
Amesema zoezi hilo ni nyeti, limeadaliwa na kufadhiliwa na kampuni maarufu nchini ya jijini Dar-es-salaam ya Mohammed Enterprises ltd ambayo mkurugenzi wake, ni mbunge wa jimbo la Singida mjini (CCM),Mohammed Gulam Dewji.
Akifafanua zaidi, amesema wagonjwa baada ya kufanyiwa upasuaji huo, hulazwa kwa mapumziko zaidi kwenye wodi ya wagonjwa wa macho ambayo ujenzi wake umegharamiwa na mbunge Dewji, pamoja na wadau wa maendeleo.
Kwa mujibu wa msaidizi wa mbunge Dewji, Hassan Mazala ambaye pia ni katibu mwenezi wa CCM manispaa ya Singida, zoezi hilo la siku tatu,linatarajiwa kugharimu zaidi ya shilingi milioni sita.
Mbunge Dewji kwa kushirikiana na taasisi na wadau mbalimbali,kwa miaka mingi iliyopita, amekuwa akiandaa na kufadhili shughuli mbalimbali za matibabu ya macho kwa wananchi wa jimbo lake na mkoa kwa ujumla.
Amekuwa akidai kwamba zoezi la upasuaji au matibabu ya macho, amekuwa akilipa umuhimu wa aina yake kwa kuamini mtu mwenye uono mzuri, anauwezo wa kutosha kupigana na maadui ujinga,umaskini na maradhi bila tatizo.Kwa hisani Ya Full Shangwe Blogu

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages