SERIKALI INAFANYA MAZUNGUMZO NA SHULE BINAFSI KUREKEBISHA VIWANGO VYA ADA ZINZOTOZWA KWA WATOTO. - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

SERIKALI INAFANYA MAZUNGUMZO NA SHULE BINAFSI KUREKEBISHA VIWANGO VYA ADA ZINZOTOZWA KWA WATOTO.

Na Mohammed Mhina
Serikali imesema inafanya mazungumzo na muungano wa Shule za binafsi hapa nchini (TAMOSO) ili kuangalia upya viwango vya ada vinavyotozwa kwa wazazi na walezi wenye watoto wanaosoma katika shule za msingi na sekondari.
Akizungumza wakati wa mahafali ya saba ya wahitimu wa elimu ya msingi kwenye shule ya St. Theresa Ukonga Jijini Dar es Salaam, Afisa Elimu Mkuu, Idara ya Elimu ya Msingi nchini Bw. Clarence Mwinuka, amesema hatua hiyo itasaidia kuweka uwiano sawa wa viwango vya ada ili kuwapa unafuu wazazi na walezi wenye watoto wanaosoma kwenye shule hizo.
Bw. Mwinuka alikuwa akizungumza kwa niaba ya Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi nchini Mh. Philip Malugo, wakati wa mahojiano maalum na Mwandishi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi nchini ambaye pia ni Afisa Uhusiano wa Jeshi la Polisi Zanzibar Inspekta Mohammed Mhina.
Amesema kuwa kutokana na kutofautiana kwa ada kati ya Shule moja na nyingine, Serikali inaendelea na mazungumzo na muungano wa shule hizo ingawa amekiri kuwa shule za binafsi zimekuwa msaada mkubwa kwa serikali katika kukuza kiwango cha elimu kwa Watanzania.
Amesemesa pamoja na msaada huo, lakini bado wananchi hasa wazazi na walezi hasa wale wa kipato cha chini wameonekana kubeba mzigo mkubwa zaidi katika kuchangia elimu kwa watoto waliopo kwenye shule hizo za binafsi hapa nchini.
Amesema majadiliano hayo yatakapokamilika Serikali inaweza kuweka viwango sawa vya ada kwa shule binafsi za msingi na za Sekondari ili kila mzazi aweze na fursa na kupeleka motto wake katika shule anayoipenda.
Hata hivyo Bw. Mwinuka amesema kuwa Serikali inaendelea na mikakati yake yakuziboresha shule zake za Msingi na Sekondari kwa kukuza viwango vya taaluma ya walimu na kuboresha mahitaji na miundombinu muhimu katika shule zake ili kusiwe na tofauti ya elimu unayotolewa katika shule binafsi na zile za Serikali.
Awali Mkuu wa Shule hiyo Sr. Amelbberga Rwezahura na Mwenyekiti wa Bodi ya Shule hiyo Bw. Wilfred Kipondya, walisema kuwa shule hiyo ina malengo ya kuhikia hatua ya juu ya utoaji wa elimu ya msingi hapa nchini kwa kuboresha miundombinu na kuhakikisha kuwa wanajenga mabweni kwa watoto wote ili kuondoa gharama za nauli na usumbufu kwa watoto kusafiri masafa marefu kwa madaladala.
Shule ya St. Theresa iliyoanza na idadi ya wanafunzi 20 wa darasa la awali, mwaka 1998 imefikia hatua hiyo baada ya mawazo na fikra za aliyekuwa Mwalimu Mkuu mwanzilishi Sr. Pepetua Mhana, za kuindeleza shule hiyo.
Sr. Mhana ndiye aliyeanzisha ujenzi wa jengo la shule hiyo yenye ghorofa mbili ambazo zinavyumba vya madarasa, ofisi za walimu na vyumba vya maabara ya sayansi.
Hivi sasa shule hiyo ina watoto 638 na imekuwa ikifaulisha kwa aslimia 100 ya watoto wote wanaosoma na kufanya mitihani ya kuingia darasa la nne na kidato cha kwanza.
Naye mmoja wa wanafunzi wanaohitimu mwaka huu darasa la saba shuleni hapo, Batuli Mhina, amesema matarajio yake atakapokuwa Sekondari atasoma kwa bidii hadi kufikia elimu ya chuo kikuu na lengo lake kubwa ni kuja kuwa Mwandhishi wa Habari.
Amesema anatamani sana kazi ya uandishi wa habari ili aje aielimishe jamii na kuwa sauti ya watoto wanaoishi mitaani kwa maisha ya kuombaomba ili nao waweze kupatiwa elimu na wajipangie malengo yao maishani.
Amesema kama wanawake wakiwezeshwa wanaweza ni vipi watoto hasa wanaoishi mitaani nao wasiwezeshwe ili waweze kupata elimu bora? Kwani amesema watoto ni Taifa la leo na wazazi wa kesho na hivyo kama mama zao wanawezeshwa nao bila kuwawezesha hawatajiweza.Habari Kwa Hisani Ya Full Shangwe Blogu

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages