Dar es Salaam Septemba 29, 2011-
Wasanii zaidi ya kumi watakaotumbuiza katika Tamasha la kwanza la Bia
Tanzania Jumamosi na Jumapili katika Viwanja vya Leaders Jijini Dar es
Salaam wameahidi kutoa burudani ya aina yake kwa watanzania.
Wakizungumza
na waandishi wa habari jana, wasanii hao na wawakilishi waliishukuru
Bia ya Kilimanjaro Premium Lager na Kampuni ya Bongo 5 kwa kuandaa
tamasha hili kubwa la kwanza na la aina yake Mkoani Dar es salaam,
Baadhi
ya wasanii na makundi yaliyohudhuria mkutano huo na waandishi wa habari
ni Chidi Benz, Msondo Ngoma, Twanga Pepeta, Akudo Impact, Canal top,
Tip Top, Ben Paul, Linex, Linah na THT ambao waliwapa wandishi wa
habari vionjo kidogo ya vitu ambavyo watavifanya katika tamasha hili.
Kilimanjaro
Premium Lager ikishirikiana na Kampuni ya Bongo 5, Alliance Francaise
na Taasisi ya Goethe wanandaa tamasha kubwa la bia la kwanza Tanzania
ambalo litafanyika katika Viwanja vya Leaders Octoba 1 na 2 mwaka huu.





No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)