Mh. Cleopa David Msuya.
Athari ambazo zinaweza kutokea kutokana na Taifa
kuendelea kuwa kizani, wananchi wanaotegemea nishati hii kama nyenzo yao ya
kujipatia kipato na uhitaji wa Nishati hiyo Mahospitalini, inaweza kutupeleka
Watanzania tukaingia kwenye vugu vugu la wananchi kutaka kuitoa Serikali iliyo
madarakani kwa njia maarufu inayoitwa 'NGUVU YA
UMMA' kama mataifa mengi ya Kiislam yalivyotokea; mfano hai ni
Misri.
Hayo yalisemwa na Mh. Msuya wakati alipokua
kwenye mjadala wa kitaifa kuhusu miundombinu, nishati na madini katika Wiki ya
Maonyesho ya Miaka 50 ya Uhuru yaliyoandaliwa na Taasisi ya Sekta Binafsi nchini
(TPSF).
KAPINGAZ Blog inawaomba wahusika walifanyie kazi haraka sana kwa maslahi ya Taifa letu.
KAPINGAZ Blog inawaomba wahusika walifanyie kazi haraka sana kwa maslahi ya Taifa letu.





No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)