Al Ahly yatolewa ubingwa wa Afrika - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

Al Ahly yatolewa ubingwa wa Afrika

Wachezaji wa Al Ahly
Wachezaji wa Al Ahly

Mabingwa mara sita wa soka barani Afrika Al Ahly wametolewa katika mbio za Ligi ya Ubingwa wa Afrika baada ya kwenda sare ya 1-1 na Esperance ya Tunisia katika mchezo wa mwisho wa kundi B.

Kwa matokeo hayo Ahly wanaweza kufikisha pointi saba na watamaliza katika nafasi ya tatu, wakati Esperance wamemaliza kileleni kwa kufikisha pointi 10. Kutolewa kwa Ahly pia kulizidi kushindiliwa baada ya klabu ya Morocco ya Wydad Casablanca ilipofungwa mabao 3-1 na Mouloudia Alger ya Algeria katika mechi nyingine ya kundi hilo. 

Wydad imemaliza ikiwa imevuna pointi saba mbele ya mabingwa hao wa Misri kwa tofauti ya mabao ya kufunga. Matokeo ya mwisho yatajulikana siku ya Jumapili wakati Enyimba ya Nigeria itaikaribisha Cotonsport ya Cameroon na Al Hilal ya Sudan itakapokuwa wageni wa Raja Casablanca ya Morocco. 

Enyimba tayari imekwishafuzu, ikiiacha Coton Sport na Al Hilal kupigania nafasi ya pili wakati Raja Casablanca itakamilisha mkiani.
Source: BBC SWAHILI

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages