MWANAMAMA
Mtafiti wa masuala ya kisayansi wa nchini Uingereza amebainika
kumtumikisha binti wa kitanzania wa miaka 21 pasipo ujira wa aina yoyote
ile kwa takribani nusu mwaka mzima.
Hayo
yamefahamika jana asubuhi katika mahakama Southwark ambapo Mwanamama
huyo Rebecca Balira anadaiwa kumtumikisha kimabavu binti Methodia
Mathias kumpikia, kumwosha pia akimtumia kama yaya wa watoto wake
watatu.
Binti
huyo wa kitanzania aliingia mkenge huo baada kulaghaiwa na mama huyo
kwamba angemlipa ujira wa pauni 96 kwa mwezi takribani Sh 300,000 za
kitanzania, lakini hakuwahi kulipwa ujira huo katu. Majaji wameelezwa
kuwa binti huyo amepokea kipigo mara kadhaa alipokuwa akihoji kuhusu
ujira wake huo.
Mahakama pia
imeelezwa kuwa binti huyo amenyang’anywa hati yake ya kusafiria na
kupigwa marufuku kuwasiliana na ndugu na familia yake aliyoiacha
Tanzania. Manyanyaso hayo yaliyodumu kwa miezi sita yalifikia kikomo
baada ya binti huyo kufanikiwa kumweleza rafikiye ambaye alipiga simu
Polisi na hatimaye suala hilo likaanza kuchunguzwa.
Kwa Habari zaidi waweza kubonya hapa Upate tukio hilo kwa kina.






No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)