MAKAMU WA RAIS ATEMBELEA MAONYESHO YA NANENANE MJINI DODOMA LEO - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

MAKAMU WA RAIS ATEMBELEA MAONYESHO YA NANENANE MJINI DODOMA LEO

Makamu wa Rais Dkt. Mohamed Gharib Bilal akiwahotubia wakazi wa Dodoma leo wakati wa maadhimisho ya utekelezaji wa mwaka wa pili wa kauli ya kilimo kwanza kwenye maadhimisho ya wakulima nanenane yanayoendelea mjini Dodoma.
Makamu wa Rais Dkt. Mohamed Gharib Bilali ( wa tatu kutoka kulia) akipata maelezo kutoka kwa Afisa Mauzo wa Pampu za kumwagiliaji aina ya Money marker kwa mikoa ya Dodoma, Iringa na Ruvuma wa Kampuni ya Kick Start International Deus Shauri( wa pili kulia) jinsi pampu hizo zilivyo saidia kuinua kipato kwa baadhi ya wakulima wanaozitimika. Afisa huyo alitoa maelezo hayo kwa Makamu wa Rais leo mjini Dodoma alioptembea maonyesho ya wakulima ya nane nane yanayoendelea.
Askari wa kikosi cha kutuliza Ghasia mkoani Dodoma Anna Makenge(kushoto) na Monica Haule(kulia)wakipata maelezo leo kutoka kwa Meneja Mawasiliano wa Mfuko wa Changamoto za Milenia Tanzania (MCA-T) Margaret Mussai juu ya shughuli mbalimbali zinzosimamiwa na mfuko huo katika kuwaletea maendeleo Watanzania. Polisi hao walipata maelezo hayo jana mjini Dodoma wakati walioptembelea banda la Wizara ya Fedha kwenye maonyesho ya wakulima nane nane yanayoendelea.
Mmoja wa watumishi wa umma wastaafu ambaye alikuwa Afisa Kilimo Mwandamzi Elias Sabuni akimuuliza Msemaji wa Wizara ya Fedha Ingiahedi Mduma(kushoto) juu hatua za uboreshaji wa stahili za wastaafu mbalimbali katika Wizara mbalimbali. Mstaafu huyo aliuza hayo leo mjini Dodoma alipotembelea banda la Wizara ya Fedha kwenye maonyesho ya nane nane yanayoendelea m jinni Dodoma Kitaifa.
Afisa Mikopo Mwandamizi wa Benki ya Uwekezaji Tanzania(Tanzania Investment Bank-TIB) Adelitha Kibuya akimweleza Makamu wa Rais Dkt Mohamed Gharib Bilali leo mjini Dodoma juu ya mikopo mbalimbali inayotolewa na Benki hiyo katika kusiadia uwekezaji katika sekta mbalimbali ili kuinua uchumi wa wananchi. Afisa huyo alitoa maelezo hayo jana mjini Dodoma wakati Makamu wa Rais alipotembelea maonyesho ya wakulima ya nane nane yanayoendelea Kitaifa mkoani hapa.
Afisa Elimu Mazingira Mkuu kutoka Idara ya Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais Martha Ngalowera akitoa maelezo kwa Makamu wa Rais Dkt Mohamed Gharib Bilali leo mjini Dodoma juu ya hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Ofisi hiyo katika kulielimisha jamii juu ya utunzaji mazingira kwa ajili ya kizazi cha sasa na kijacho. Makamu wa Rais alitembelea maonyesho ya wakulima ya nane nane yanayoendelea mjini Dodoma ili kujionea shughuli mbalimbali zinazoendelea.
Habari Kwa HIsani Ya John Bukuku - Full Shangwe Blogu 

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages