MBUNGE WA MVOMERO AINGILIA KATI MGOGORO WA ARDHI KIPERA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

MBUNGE WA MVOMERO AINGILIA KATI MGOGORO WA ARDHI KIPERA

 Mbunge wa Jimbo la Mvomero, Amos Makala, akizungumza na wananchi wa Kitongoji cha Kinyenze, Kijiji cha Kipera, Tarafa ya Mlali, Wilaya ya Mvomero, Morogoro mwishoni mwa wiki katika harakati za kutatua mgogoro wa ardhi uliopo kijijini hapo, kufuatia mwekezaji  Raia wa kigeni  kuuziwa eneo kubwa la ardhi  na kumega sehemu ya mashamba yao na kufunga barabara, shule na kubomoa baadhi ya vyoo vya wakazi wa kijiji hicho. Picha na Mroki Mroki
 Mbunge wa Jimbo la Mvomero, Mkoani Morogoro, Amos Makala (kushoto)  akikagua uzio uliowekwa na Kampuni ya Tanbreed Poultry Limited inayomilikiwa na Mzungu aliyenunua shamba Kitogoji cha Kinyenze, Kijiji cha Kipera, Tarafa ya Mlali, Wilaya ya Mvomero na kuzua mgogoro mkubwa wa mipaka baina yake na wananchi wa eneo hilo. Anayemuongoza ni Said Ahmad mkazi wa Kinyenze.
Wananchi wa Kitongoji cha Kinyenze, Kijiji cha Kipera, Tarafa ya Mlali, Wilayani Mvomero, wakiwa katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na Mbunge wa Jimbo la Mvomero, Amos Makala aliyefika kijijini hapo mwishoni mwa wiki kufuatilia mgogoro wa ardhi ulipo kati ya wananchi hao na mwekezaji raia wa kigeni aliyenunua shamba kijijini hapo na kuweka uzio na kufunga njia na mashamba yao.
***********************************************************
*Atoa wiki moja maofisa ardhi kumaliza tatizo au kutinga Mahakamani

Na Mroki Mroki, Mvomero

MBUNGE wa jimbo la Mvomero, mkoani Morogoro, Amos Makala, ameingilia kati mgogoro wa ardhi uliopo baina ya Mwekezaji na Wananchi wa Kitongoji cha Kinyenze , Kijiji cha Kipera, Tarafa ya Mlali , Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro.

Akizungumza mwishoni mwa wiki Kijijini hapo, Makala aliyeambatana na Ofisa Ardhi wa Wilaya hiyo, Majaliwa Jaffari ameiagiza idara ya ardhi kuchukua hatua za haraka na dharula kutatua mgogoro huo kabla ya kuibuka kwa machafuko ya uvunjifu wa amani.
Kwa Habari Zaidi <<< BOFYA HAPA >>>

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages