Mbunge wa Munduli, Edward Lowassa(Katikati)akizungumza na
waandishi wa habari kwenye viwanja vya bunge mjini Dodoma jana,
walipotaka kupata maoni yake kuhusu uamuzi wa Rostam Aziz kujiuzulu
nyadhifa zake za ubunge wa Igunga na ujumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM
hata hivyo Edward Lowassa ameeleza kushtushwa na tukio hilo.
Hata hivyo, Lowassa ambaye naye
amekuwa akitajwa katika orodha ya watu watatu wanaopaswa kuachia nafasi
zao za uongozi CCM katika kile kinachoitwa chama kujivua gamba,
alipoulizwa kuhusu taarifa za yeye kufuata njia ya mshirika wake huyo
alijibu: "Siku ikifika nitatoa uamuzi na nitajibu wakati ukifika."
Lowassa alikuwa akijibu maswali ya
waandishi wa habari katika Viwanja vya Bunge mjini Dodoma, kuhusu
alivyopokea uamuzi huo wa Rostam na kama yuko tayari kufuata mfano na
njia hiyo ya kujiuzulu nyadhifa zote ndani ya CCM.
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)