Naibu
katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma HAB Mkwizu
(kushoto) akiongea na waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu
maadhimisho ya siku ya utumishi wa Umma ya Umoja wa Mataifa na Afrika
ambayo itafanyika kuanzia tarehe 20 hadi 23 Juni mwaka huu katika
viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es Salaam. Kulia ni Msemaji wa
Zamaradi Kawawa.Mkutano huo ulifanyika leo katika ukumbi wa mikutano
uliopo makao makuu ya ofisi hizo.
Baadhi
ya waandishi wa Habari wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais
Menejimenti ya Utumishi wa Umma HAB Mkwizu (hayupo pichani) wakati
akiongea nao kuhusu maadhimisho ya siku ya utumishi wa Umma ya Umoja wa
Mataifa na Afrika ambayo itafanyika kuanzia tarehe 20 hadi 23 Juni
mwaka huu katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es Salaam.Mkutano
huo ulifanyika leo katika ukumbi wa mikutano uliopo makao makuu ya
ofisi hizo.
Baadhi
ya wakurugenzi wa Idara kutoka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa
Umma wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa ofisi hizo HAB Mkwizu (hayupo
pichani) wakati akiongea na waandishi wa Habari kuhusu maadhimisho ya
siku ya utumishi wa Umma ya Umoja wa Mataifa na Afrika ambayo
itafanyika kuanzia tarehe 20 hadi 23 Juni mwaka huu katika viwanja vya
mnazi mmoja jijini Dar es Salaam.Mkutano huo ulifanyika leo katika
ukumbi wa mikutano uliopo makao makuu ya ofisi hizo.
---
NA MAGRETH KINABO –MAELEZO
TANZANIA
imechaguliwa kuwa mwenyeji wa maadhimisho wa wiki ya Utumishi wa Umma
ya Umoja wa Mataifa na Afrika yatakayofanyika jijini Dares Salaam
kuanzia Juni 20 hadi Juni 23, mwaka huu.
Hayo yalisemwa leo na Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya
Utumishi wa Umma, HAB Mkwizu wakati akizungumza na waandishi wa habari
jijini Dares Salaam. Alisema
maadhimisho hayo ambayo yanatarajiwa kushirikisha washiriki zaidi ya
400, taasisi za hapa nchini 160 na kutoka nje ya nchi zaidi ya 50.
Mkwizu aliongeza kuwa maadhimisho hayo yatakuwa ni ya sehemu mbili
yaani makongamano yatakayofanyika Mlimani City na maonyesho katika
viwanja vya MnaziMmoja.
Alisema mgeni rasmi katika maadhimisho hayo anatarajiwa kuwa Msaidizi
wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anyeshughulikia Maendeleo ya
Utumishi wa Umma,Haiyan Qian.
Pia katika makongamano kutakuwepo wageni mbalimbali.
Pia yataambatana na maadhimisho ya shughuli za maonyesho ya wiki ya
utumishi wa umma ya barani Afrika, yatakayoanza Juni 16,mwaka huu hadi
Juni 23,mwaka huu. Kauli
mbiu ya katika makongamano ni ‘Mabadiliko na Ubunifu wa Viongozi katika
Utumishi wa Umma Utaleta Maisha Bora’, wakati ya maonyesho ni ‘Mkataba
wa Kanuni na Msingi ya Utumishi wa Umma Barani Afrika ni chachu ya
Kuimarisha Utoaji Huduma Bora kwa Umma’, ‘Miaka
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)