MPAMBANO WA MACHINGA NA MGAMBO JIJINI DAR - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

MPAMBANO WA MACHINGA NA MGAMBO JIJINI DAR

Mgambo wakivunja baadhi ya maboksi ambayo hutumiwa na watengeneza saa na wachonga mihuri katika makutano ya mitaa ya Msimbazi na Uhuru leo jijini.
WAFANYABIASHARA ndogondogo katika soko la Kariakoo, jijini Dar es Salaam, bado wanakumbana na adha kutokana askari wa jiji kuwachukulia vitu vyao kwa nguvu na kutoweka navyo.

Wakizungumza leo na kamera yetu, wafanyabiashara hao kwa nyakati tofauti wamesema  kuwa hali si shwari kwao kutokana na kuburuzwa mara kwa mara na mgambo wa jiji.

Gari la kuzolea taka likiwa limezungukwa na uchafu jirani na soko la Kariakoo.  Wafanyabiashara wamedai kuwa mlundikano huo wa uchafu unatoa harufu kali inayowafanya kufanya shughuli zao kwa taabu pia kuhatarisha afya zao, hivyo wameiomba Halmashauri ya Manispaa Ilala kushughulikia kero hiyo haraka.
 
Mama wa Kimaasai ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja akiondoka eneo la kuuzia biashara zake baada ya askari wa jiji kusomba meza yake ya biashara  na bidhaa zake za asili eneo la Kariakoo, leo.

PICHA/HABARI NA HARUNI SANCHAWA /GPL.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages