Pages

‘MO DEWJI’ ATOA MCHANGO WALE KATIKA MASHINDANO YA RIADHA YA AFRIKA MASHARIKI NA KATI

 Mkurugenzi wa Radio One Stereo Deogratius Rweyunga akitoa shukrani kwa kampuni ya MeTL kwa kuona umuhimu wa kuchangia ili kufanikisha mashindano hayo na kuzitaka kampuni zingine kuiga mfano huo.
 Afisa Uhusiano wa MeTL Esther Dotto akielezea jinsi Mheshimiwa Mbunge wa Singida Mjini alivyoguswa na Tanzania kuwa mwenyeji wa mashindano hayo na kuahidi kuendelea kushiriki zaidi katika kuhakikisha Tanzania inafanikiwa kimichezo.
Afisa Uhusiano wa Kampuni ya MeTL ambaye pia ni msaidizi wa Mh. Mohammed Dewji (Mb) Esther Dotto akikabidhi mchango katoni 42 za maji safi ya kunywa ‘ MAISHA’ yanayotengenezwa na Kampuni ya A-ONE Products and Bottlers ambayo ni moja ya makampuni ya MeTL kwa Mkurugenzi wa Radio One Deogratius Rweyunga kwa ajili ya maandalizi ya mashindano ya riadha ya Afrika Mashariki na Kati yatakayofanyika katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 3-4 June, 2011.
Mh. Mohammed Dewji Mbunge wa Singida Mjini.“Ni vyema sisi kama watanzania tukachangia kukuza maendeleo yetu wenyewe katika michezo, na si katika soka peke yake, bali kwa michezo yote kwa ujumla”
Katoni za maji safi ya kunywa aina ya MAISHA yanayotengenezwa na moja ya kampuni ya MeTL yaliyokabidhiwa kama mchango kwa ajili ya mashindano hayo.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)