Mwenyekiti wa WAMA, Mama Salma Kikwete akisalimiana na wadau waliohudhuria katika mkutano huo.
Mwenyekiti
wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) Mama Salma Kikwete
akihutubia katika mkutano wa wadau mbali mbali wa shirika la
CAMFEDTanzania, mkutano uliofanyika leo katika ukumbi wa Karimjee
jijini Dar es Salaam. Akihitubia katika mkutano huo Mama Salma Kikwete
alisema kuwa WAMA ipo tayari kushirikiana na wadau mbali mbali katika
kumsaidia mwanamke kiuchumi. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa
CAMFED Tanzania Msaada Daudi Balula. Shirika la CAMFED Tanzania
limejikita katika kutoa huduma zake katika Wilaya kumi za Tanzania
ambazoni ni Kibaha,Kilolo ,Iringa Vijijini,Rufiji, Bagamoyo,Morogoro
Vijijini, Kilombero, Pangani na Handeni.
Wadau wakiwa katika mkutano huo.Picha na Victor Makinda
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)