MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA

NANI ATATUOKOA?
Kutokana na uhaba wa nishati ya gesi kukosekana katika maeneo mbalimbali hasa vijijini, wananchi wamelazimika kutumia kuni kwa ajili ya mahitaji ya nyumbani, kama mwanamke huyo alivyokutwa juzi Wilayani Kilombero, mkoani Morogoro akiwa amejitwisha mzigo wa kuni.
 HAPA AKIWA AMELALA KWA AJILI YA NJAA KALI.
Mtoto, Daudi Lafa Chengula, aliyetokea Mkoa wa Iringa kuja Dar es Salaam bila kuwa na ndugu yeyote wa kumsaidia, kwa sababu ya maisha magumu vijijini akihojiwa na wasamalia wema katika eneo la hotel ya Blue Pearl jijini Dar es Salaam jana.
 
Watoto, wakiwa wamebeba chupa za maji walizookota Ubungo jijini Dar es Salaam jana, katika kituo cha mabasi yaendayo mkoani kwa ajili ya kuuza na kupata pesa za mahitaji.
Mwendesha baiskeli yenye matairi matatu (guta), akiwa amebeba abiria aliyekaa bila kuhofia usalama wa maisha yake katika eneo la Keko, Dar es Salaam.

Mwendesha pikipiki akiendesha pikipiki yake iliyosheheni mikate na kushindwa kuona nyuma jambo linalohatarisha maisha yake kwani anaweza kugongwa na gari linalotoka nyuma yake.
 
Na Janneth Tabasamu

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages