KIWANDA CHA SERENGETI CHA MJINI MOSHI CHAANZA UZALIASHAJI RASMI - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

KIWANDA CHA SERENGETI CHA MJINI MOSHI CHAANZA UZALIASHAJI RASMI


Mkurugenzi wa Kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) Richard Wells akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa usamabazaji wa bia za Serengeti Lager, zinazozalishwa na kiwanda hicho kipya katika mji wa Moshi mkoani Kilimanjaro na vitongoji vyake ikiwemo na mikoa ya jirani ,uliofanyika jioni ya Jana ambapo uzinduzi huo uliambatana na msafara mkubwa wa magari uliozunguka katikati ya mji wa moshi huku msafara huo ukiongozwa Mkurugenzi huyo, Richard Wells,sambamba na wafanyakazi wa kampuni hiyo,shamra shamra hizo zilinogeshwa zaidi wakati wafanyakazi wa kampuni hiyo walipoamua kugawa bure kinywaji hicho cha Serengeti katika maeneo mbalimbali.
Mkurugenzi wa Kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) Richard Wells akizungumza mbele ya baadhi ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali wakiwemo wafanyakazi wa kiwanda hicho,wakati wa uzinduzi rasmi wa usambazaji wa kinywaji hicho,uliofanyika jioni ya jana,kulia kwa Mkurugenzi ni Mkuu wa Mahusiano na jamii- Moshi Bwana Mandala akisikiliza kwa makini.
Mkurugenzi wa Kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) Richard Wells wakiteta jambo na Mkuu wa Mahusiano na jamii (Moshi), Bwana Mandala.
Pichani kati ni Mkurugenzi wa Kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) Richard Wells akisalimiana na mdau mkubwa wa kinywaji cha Serengeti Lager,Loui Kifwanga aliyefika pia kushuhudia uzinduzi rasmi uliofanyika jioni ya jana kiwandani hapo,na kushoto ni Mkuu wa Mahusiano na jamii (Moshi), Bwana Mandala
Pichani kati alienyoosha mkono juu ni Mkurugenzi wa kampuni ya Serengeti Breweries (SBL),Richard Wells akipiga picha ya pamoja na wafanyakazi wa idara ya usambazaji kabla ya kuondoka kiwandani hapo jioni ya jana
Pichani kulia ni Meneja wa kinywaji cha Serengeti Lager,Allan Chonjo wakifurahia na mdau wa mwingine wa kampuni hiyo kuzinduliwa rasmi kwa kiwanda hicho katika mchakato mzima wa kusambaza kinywaji chake.
Meneja wa Kinywaji cha Serengeti Lager,Allan Chonjo pamoja na wafanyakazi wenzake wakishangilia mara baada ya uzinduzi rasmi kufanyika jioni ya jana kiwandani hapo,mjini Moshi.
Gari ikitoka kiwandani hapo ikiwa tayari imesheheni mzigo tayari kwa kuwapelekea wateja,huku wafanyakazi wa kampuni hiyo wakitia baraka zao kwa kupiga makofi kwa pamoja.
Baadhi ya wafanyakazi wa Serengeti wakiwa bize jioni ya jana mara baada ya uzinduzi rasmi.
Mlima Kilimanjaro uonekanavyo kwa nje ya kiwanda hicho.
Mmoja wa wafanyakazi wa kampuni hiyo akipakia bia katika gari kwa kutumia mashine maalum ya kunyanyulia mizigo kiwandani hapo,tayari kwa kuwasambazia wateja wao popote pale.
Pichani ni msafara wa magari ukikatiza katikati ya mji wa Moshi jioni ya jana kuashiria kuwa tayari bia aina ya Serengeti imeanza rasmi kuzalishwa ndani ya mji huo kwa wateja wao.Magari hayo yalikuwa yamepambwa kwa maandishi makubwa 'Kiwanda chetu,Bia Yetu !
Huu ndiyo muonekano wa kiwanda cha Kampuni ya bia ya Serengeti mjini Moshi katika mkoa wa Kilimanjaro kilichozindua rasmi usambazaji wa bia zake mara baada ya kuanza uzalishaji jioni ya jana.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages