KAMBARAGE, KAWAWA NA KAWAWA KISA CHA MAPACHA WATATU - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

KAMBARAGE, KAWAWA NA KAWAWA KISA CHA MAPACHA WATATU


" Kambona , ah, ah!
Kambona, ameolewa!
Wapi?
Uko Ulaya!
Wivu?
Wamkereketa!"

Utotoni nilipata kuwasikia kaka zetu wakiimba wimbo huo wa mchakamchaka. Nikiwa shuleni nimesoma sana habari za siasa za wakati huo. Bado naendelea kusoma na kujifunza. Katika kusoma kwangu nimeona, kuwa suala la ugomvi wa Oscar Kambona na Julius Nyerere alikuwa rahisi vile kama tulivyoambiwa na hata kuimbiwa. Simulizi za Oscar Kambona zinabaki kwa wengi kuwa ni za upande mmoja.

Hakika, si wengi wenye kufahamu nini hasa kiliwatokea marafiki watatu hawa; Julius Nyerere, Oscar Kambona na Rashid Kawawa. Kizazi hiki cha sasa cha Watanzania kinaweza kunufaika sana na uelewa wa yaliyojiri katika harakati za kisiasa za wakati huo zilizopelekea uhuru wa Tanganyika na baadae Oscar ' Kujivua' gamba kwa kutokubaliana na rafiki yake Julius juu ya Azimio la Arusha. Kuna maswali ya kujiuliza; Je, ugomvi wa Oscar na Julius ulianzia kwenye Azimio au kabla ya hapo? Je, umma ulipotoshwa juu ya nini kilichotokea? Ikumbukwe, Oscar na Julius walikuwa marafiki wa kushibana kiasi cha Julius kuwa ' Mpambe' wa Oscar kwenye ndoa yake iliyofanyika London. Je, Rashid alichangia kwenye ' kutoswa' au ' kujitosa' kwa Oscar. Kwamba Oscar aliona hakupata kuungwa mkono na Rashid. Je,  Oscar alifanya makosa kwa kuondoka nchini badala ya kubaki na kupambana kwa hoja na rafiki yake Julius?

Je, nianze kuwasimulia machache niliyojitahidsi kuyajua, au niwaache kwanza wengine msimulie mnayoyajua, maana, kuna wanaodhani wanajua na kuna wanaojitahidi kujua. Mie niko kwenye kundi  hilo la pili!

Na
 Maggid Mjengwa

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages