MAADHIMISHO YA SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI,JIJINI DAR LEO - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

MAADHIMISHO YA SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI,JIJINI DAR LEO

Baadhi ya wafanyakazi wa Ofisi ya Makamu wa Rais, wakipita na bango lenye ujumbe mbele ya mgeno rasmi Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Mecky Sadiki, jukwaa kuu wakati wa sherehe za maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) zilizofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam leo. Sherehe hizo Kitaifa zilifanyika Mkoani Morogoro ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete.
Wafanyakazi wa Ofisi ya Makamu wa Rais, wakipita jukwaa Kuu huku wakishangilia na kufurahia, wakati wa sherehe za maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) iliyofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja.
Maandamano yakiendelea kuelekea Viwanja vya Mnazi Mmoja.
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mecky Sadiki (katikati) akiwa na baadhi ya viongozi wa wilaya ya Ilala jukwaa kuu wakati akipokea maandamano ya wafanyakazi katika sherehe hizo.
Wafanyazi wa Ofisi ya Makamu wa Rais, wakishiriki katika maandamano hayo kuelekea Viwanja vya Mnazi Mmoja katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Duniani.
Baadhi ya wafanyakazi wa ofisi ya Makamu wa rais wakiwa wamepumzika wakati wakisubiri kuingia katika viwanja vya Mnazi mmoja baada ya kuwasili mgeni rasmi Kamimu Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, wakati wa sherehe za maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Duniani, (Mei Mosi) zilizofanyika kwenye uwanja huo.
Mmoja wa wafanyakazi ambaye hakuweza kufahamika jina lake, akiwa bize kushona kitambaa cha uzi wakati akiwa kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja.
Askari Magereza wakiongoza maandamano hayo kuelekea ndani ya Viwanja vya Mnazi Mmoja.
Wengine wakijifariji kwa kupiga stori wakati wakimsubiri mgeni rasmi kuingia katika viwanja vya Mnazi mmoja Dar es Salaam leo tayari kwa kuanza maandamano ya kupita mbele ya mgeni huyo rasmi.
Gari la Maliasili likipita huku likiwa na mapambo ya ngozi za wanyama wakali kama Chui na wengineo katika maadhimisho hayo.
Khalili Ibrahim akipozi na bosi wake Eng. Chalamila, wakiwa kwenye sherehe hizo.
Wafanyakazi wakiandamana kuelekea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam leo, wakati wa sherehe jizo.
Katika sherehe hizo pia yalitaka kutokea maafa baada ya moja ya banda hili linaloonekana pichani kuvunjika na kutaka kuwafunika watu waliokuwap eneo hilo wakijikinga mvua.
Wafanyakazi wa Tawi la Kampuni ya Tuico, wakipita mbele ya Jukwaa kuu na mabango yao yenye Ujumbe, wakati wa sherehe hizo.
Wengine hawakuweza kupata mahala pa kupumzika kutokana na uwingi wa watu waliohudhulia sherehe hizo leo, hivyo iliwalazimu kusimama muda wote.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages