WASHIRIKI WA MISS DAR CITY CENTER WAANZA MAZOEZI LAMADA HOTEL - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

WASHIRIKI WA MISS DAR CITY CENTER WAANZA MAZOEZI LAMADA HOTEL

Pichani ni wanyange 18 ambao wamejitokeza kushiriki kwenye shindano la kumsaka Miss Dar City Centre 2011.Bongoweekend ilipata fursa ya kuwatembelea na kuwaona mashaallah wamo miongoni mwao ambao huenda wakafika mbali.

Shindano hilo linaratibiwa na Fetty Intertainment chini ya Mkurugenzi Fetty Mgovano ambaye nayeye alikuwa mshiriki wa Miss Tanzania 2005.

Shindano la Miss Dar City Centre litafanyika katika viwanja wa Lamada Ilala Dar es salaam Mei 13 mwaka huu.

Warembo hao wanafundwa na Rehema Uzuia ambaye alikuwa Miss Ruvuma pia alishiriki katika shindano la Miss Tanzania 1999 akisaidiana na Miss Morogoro 2003 Angel Michael.

Mbai ya waalimu hao pia mnenguaji wa bndi ya TOT kwa sasa Bokilo ambaye aliahi kung'ara katika bendi ya Twanga ndiye anafundisha kucheza shoo.

Mlezi wa warembo hao nikaambiwa ni Fatma Issa.

Fetty alisema kuwa mchujo utafanyika na kwa sasa bado anapokea warembo tarehe ya mchujo kutangazwa baadaye.
Habari/Picha Na BongoWeekend

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages