
Katibu Mkuu wa Chama cha (Tanzania Association of Managers nad Owners of Non -Government Schools and Colleges) ndugu Benjamin Nkonya kushoto na kulia ni Mwenyekiti wa Chama hicho ndugu Jerry Nyabululu wakizungumza na Waandishi wa Habari ambao hawapo kwenye picha ,kwenye Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) jijini Dar es Salaam leo kuhusu matoke ya kidato cha nne mwaka 2010 yafutwe, na Mitihani isahihishwe upya , kwani utaratibu wa usahishaji wa mitihani hiyo ulichukua muda mfupi kwa sababu ya Bajeti ya Baraza la Mitihani kuwa finyu kwani vyanzo vya mapato vimepungua ni baada ya Serikali kuondoa Ada ya Mitihani kwa Shule za Serikali,hivyo kufanya Baraza kuwa na uwezo mdogo wa kusimamia kazi ngumu ya kusahihisha Mitihani ya Nchi nzima.Picha na Anna Itenda -Maelezo

No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)