KINANA ASEMA CCM HAIKO TAYARI KUBURUZWA NA WAPINZANI, IKO TAYARI KUKOSOLEWA KWA HOJA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

KINANA ASEMA CCM HAIKO TAYARI KUBURUZWA NA WAPINZANI, IKO TAYARI KUKOSOLEWA KWA HOJA

1Msafara wa Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ukielekea Kata ya Dutwa Wilayani Bariadi Mkoa mpya wa Simiyu ambako ametembelea mashina na miradi kadhaa ikiwa ni pamoja na kuhimiza utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya Chama hicho, Katibu Mkuu Kinana ameongozana na Katibu wa Itikadi , Siasa na Uenezi wa CCM Ndugu Nape Nnauye pamoja na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Simiyu na wilaya ya Bariadi akiwemo Mbunge wa jimbo la Bariadi Magharibi Mh Andrew Chenge, Katibu Mkuu huyo anamalizia ziara yake katika mkoa wa Simiyu kesho kwa kufanya ziara katika jimbo la Busega na keshokutwa ataanza ziara katika mkoa wa Mara akianzia Wilaya ya Bunda, Katika mkutano wa hadhara uliofanyika leo kwenye soko la Dutwa Abdulrahman Kinana amesema Chama cha Mapinduzi hakitakubali kuburuzwa na wapinzani ila kiko tayari kukosolewa kwa hoja na si kwa matusi, kejeli na vitisho vya wanasiasa. 3 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wa pili kutoka kulia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu Mh. Dk Titus Kamani wakishirikiana na wananchi kusogeza matofari katika eneo itakapojengwa nyumba ya mwenyekiti wa shina namba 12 Isenge kijiji cha Igaganulwa Kata ya Dutwa ambapo Katibu Mkuu huyo amfanya harambee na kukusanya michango mbalimbali kwa ajili ya kununulia vifaa vya ujenzi wa nyumba hiyo. 4Mbunge wa Jimbo la Bariadi Magharibi Mh. Andrew Chenge wa nne kutoka kulia ni Pascal Mabiti Mkuu wa mkoa wa Simiyu wa tano wakishiriki katika zoezi la kubeba matofali kwa ajili ya ujenzi wa nyumba hiyo ya mwenyekiti wa shina. 6Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kulia na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi wakishiriki kuchimba msingi kwa ajili ya ujenzi wa nyumba hiyo inayojengwa katika kitongoji cha Isenge kata ya Dutwa. 7Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi Nape Nnauye akiwa amekaa pamoja na wananchi katika mkutano wa shina namba 12 Isenge kata ya Dutwa. 8Wananchama wa CCM shina la Isenge wakimsikiliza Katibu Mkuu hayupo pichani. 9Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kulia akishiriki kula chakula cha kiasili cha kisukuma kinachoitwa Michembe, kutoka kushoto ni Mh. Andrew Chenge Mbunge wa jimbo la Bariadi Magharibi, Pascala Mabiti Mkuu wa mkoa wa Simiyuna Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu Dk. Titus Kamani wakishiriki kula chakula hicho. 10Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi Nape Nnauye akila wali pamoja na wananchi katika kata hiyo 12Wakina mama wakiendelea na biashara zao katika soko la Kata ya Dutwa ambalo limejengwa na Serikali kwa kushirikiana na wananchi pamoja na mbunge wa jimbo hilo. 13Biashara zikiendelea sokoni hapo. 14Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kulia kushoto akiongozana na Mbunge wa jimbo la Bariadi Magharibi Mh. Andrew Chenge wakati akikagua soko hilo. 15Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiulizia bei ya Dagaa kwa Zawadi Malina Mchuuzi wa Dagaa katika soko hilo. 16Daud Njalu Silanga Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Simiyuakinunua Kabichi kutoka kwa Marietha Maiko mchuuzi wa mbogamboga katika soko hilo lililopo kata ya Dutwa Bariadi. 18Wananchi wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana hayupo pichani wakati akizungumza katika soko la Dutwa. 19Mh. Andrew Chenge Mbunge wa jimbo la Bariadi Magharibi akizungumza na wananchi katika soko hilo. 20Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana hayupo pichani akipokelewa na wananchi kwa kunyanyua bendera juu ikiwa ni ishara ya ukaribisho rasmi kwa Katibu Mkuu huyo. 21Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kujenga ukuta wa choo cha shule katika shule ya sekondari ya Malambo katika halmashauri ya mji ya Bariadi.(PICHA NA KIKOSI KAZI CHA FULLSHANGWE-BARIADI SIMIYU)

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages