Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia mkutano wa hadhara katika viwanja vya sabasaba mjini Bariadi leo katika ziara yake ya mwisho kwenye wilaya hiyo mkoani Mkoani Simiyu ambapo kesho atamalizia katika jimbo la Busega na kwenda moja kwa moja mkoani Mara tayari kwa kuanza ziara nyingine ya siku sita mkoani humo. Nape nnauye katibu wa NEC Itikadi, Siasa na uenezi akiwahutubia wananchi wa Bariadi katika mkutano huo uliofanyika mjini Bariadi leo. Nape nnauye katibu wa NEC Itikadi, Siasa na uenezi wa pili kutoka kulia akifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana hayupo pichani wakati alipokuwa akiwahutubia wananchi katika viwanja vya Sabasaba mjini Bariadi leo, kulia ni Dk Titus Kamani Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu na kutoka kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Bariadi Erasto Sima na Pasacl Mabiti Mkuu wa mkoa wa Simiyu. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikabidhi pikipiki kwa Doto Nchege mwenyekiti wa kikundi cha waendesha bodaboda wa mjini Bariadi baada ya mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Sabasaba mjini Bariadi Waendesha bodaboda wakiondoka na pikipiki zao mara baada ya kukabidhiwa na katibu mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana leo.
Post Top Ad
Responsive Ads Here
Post Bottom Ad
Responsive Ads Here
Author Details
Lukaza Blog is a resources blog providing high quality articles with premium topics and well drafted. The main mission of Lukaza Blog is to provide the best quality articles which are relevance, original, truth and education materials designed and perfectlly to deliver best result for your knowledge and understanding of new things.
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)