ZANZIBAR HALI BADO NI TETE MABOMU YA MACHOZI YAENDELEA KURINDIMA TOKEA JANA JIONI HADI ASUBUHI YA LEO - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

ZANZIBAR HALI BADO NI TETE MABOMU YA MACHOZI YAENDELEA KURINDIMA TOKEA JANA JIONI HADI ASUBUHI YA LEO

Hizi ni baadhi ya vurugu zilizotokea jana Mjini Zanzibar huku mabomu ya machozi yakirindima na kuendelea kupigwa na polisi wakati wa vurugu zilizoshababishwa na kundi kubwa la watu kwenda kuvamia kituo cha polisi ili kushinikiza kiongozi wao aliyeshikiliwa na jeshi la polisi aachiwe huru
Picha askari wa kutuliza ghasia akiwa tayari kwa mapambano n awananchi wa zanzibar ambao inasemekana walivamia kituo cha polisi wakiwa na silaha za jadi kama vile rungu na mapanga
Hali tete bado inaendelea asubuhi ya leo mjini zanzibar huku polisi wakiwatawanya wananchi wa zanzibar lakini wananchi hao wanazidi kuongezeka kwa kutaka kiongozi wao kuachiwa huru na polisi ambapo alikamatwa jana na wananchi hao kuvamia kituo cha polisi jana jioni na hatimaye polisi kutumia mabomu ya machozi tokeaa jana jioni hadi asubuhi ya leo
Wananchi wa Zanzibar wakiwa kwenye maandamano wakati wakielekea kituo cha polisi na kabla machozi ya mabomu hayajaanza kulipuliwa na askari.Picha Zote na  Abdulaziz El Shuwehdy

JANA JIONI KUNDI KUBWA LA WATU WANAOLIUNGANISHA KUNDI LIFAHAMIKALO KWA JINA LA UAMSHO,AMBALO LIMEKUWA LIKIUPIGA VITA MUUNGANO WA TANZANIA NA ZANZIBAR,LILIVAMIA KITUO KIKUU CHA POLISI CHA MADEMA KISIWANI HUMO JIONI YA JANA NA KUSABABISHA VURUGU KUBWA,WAKITAKA KUACHILIWA KWA KIONGOZI WAO ALIEKAMATWA JIONI YA JANA KWA KUONGOZA MHADHARA BILA YA KUWA NA KIBALI CHA SERIKALI.
HALI HIYO IMESABABISHA VURUGU KUBWA KITUONI HAPO HUKU ASKARI POLISI WA KITUO HICHO WAKILAZIMIKA KUTUMIA MABOMU YA MACHOZI ILI KUWATAWANYA WATU HAO AMBAO WENGI WAO WAKO NA SILAHA ZA JADI AMBAZO NI MARUNGU,MAPANGA NA MAWE ILI KUPAMBANA NA ASKARI POLISI KITUONI HAPO VURUGU HIZO ZIMEENDELEA TENA ASUBUHI YA LEO.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages