Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akimshukuru mwenyeji wake Spika
wa Bunge la Japan Mhe. Takahiro Yokomichi na Ujumbe wake wa Wabunge
wanaounda kamati inayoshughulikia Maswala ya Afrika kwa mwaliko
waliompatia yeye na Ujumbe wa wabunge Kutoka Bunge la Tanzania kuja
Japan kubadilishana uzoefu katika maswala ya Kibunge pamoja na
kuimarisha ushirikiano kati ya mabunge haya mawili. Kulia kwa Mhe.
Makinda ni Mhe. Godfrey Zambi na Mhe. James Lembeli walioambatana Na
Mhe. Spika katika Ziara hiyo. Picha na Owen Mwandumbya
--
Na Mwandishi wetu, Tokyo Japan
Spika
wa Bunge Mhe. Anne Makinda amesema, Tanzania inajivunia uhusiano mzuri
kati yake na Japan. Akizungumza katika majumuisho ya ziara yake nchini
Japan, Mhe. Makinda amesema, Bunge la Tanzania linaishukuru Serikali
ya Japan na Bunge lake kwa kumwalika yeye na Ujumbe wa Wabunge kutoka
Tanzania kuja kujifunza maswala Mabalimbali ya Kibunge ikiwa ni pamoja
na kukuza demokrasia ya kibunge baina ya nchi hizi Mbili.
Amesema,
Pamoja na Japan kupitia katika hali ngumu ya kulipuliwa kwa miji yake
miwili ya Hiroshima na Nagasaki wakati wa Vita kuu ya Pili ya Dunia,
Matetemeko ya mara kwa mara na mafuriko ya Tsunami, lakaini bado uchumi
wake haujayumba kiasi kwamba sasa waJapan wameweza kusima imara
kuijenga nchi yao.
Mhe.
Makinda amesema Demokrasia safi na Siasa imara za Japan ni mfano tosha
na fundisho kwa Tanzania ambapo hivi sasa katika kuimarisha uhusiano
huu wa Kibunge, mabunge haya mawili yatabadilishana uzoefu katika
maeneo mbalimbali kwa lengo la kuimarisha utendaji kazi wa Bunge la
Tanzania.
“
Nchini yenu mmekomaa sana katika Demokrasia, ikiwa ni pamoja na
uendeshaji wa shughuli za Kibunge, sisi kama watanzania tuna mengi
sana tungependa kujifunza kutoka kwenu, leo mmenialika na ujumbe wangu
kutembelea Bunge lenu, lakini napenda kusema huu uwe ndio mwanzo wa
kuimarisha uhusiano wetu, ikiwezekana hata kamati zetu za Bunge zipate
fursa ya kujifunza kutoka kwenu. Ziara za namna hii zitatusaidia
kupanua uelewa wetu katika maswala ya Kibunge“ alisema Mhe. Makinda.
Katika
kuhakikisha kuwa Bunge la Tanzania linaimarisha uhusiano wake na Bunge
la Japan, Spika Makinda ametoa Mwaliko maalum kwa Spika wa Bunge la
Japan Mhe. Takahiro
Yokomichi kuja kutembelea Tanzania ikiwa ni pamoja na kubadilishana
uzoefu na wabunge wengine kutoka Bunge la Tanzania.
Mhe.
Makinda amesema, Bunge la Tanzania linayo kamati ya Bunge
inayoshughulikia maswala ya mambo ya Nje na uhusiano wa Kimataifa, hivyo
ni fursa pekee ya kamati hii na wenzao kutoka Bunge la japan
kushrikiana kwa karibu kuhakikisha ushirikano huu unakuwa imara na
endelevu.
Akimshukuru
Mhe. Makinda kwa kukubali mwaliko wake, Spika wa Bunge la Japan Mhe.
Takahiro Yokomichi, amesema nchi yake iliichagua Tanzania miongoni mwa
nchi za Afrika hususani Africa Mashariki kutembelea Bunge la Japan kwa
kuwa ni nchi yenye demokrasia safi na siasa zake zinaimarika kila kukich
na kuifanya Japan kuvutiwa na maendeleo hayo katika Bunge la Tanzania.
Mhe.
Yokomichi amesema huu ni mwanzo wa ushirikiano muhimu baina ya Mabunge
haya mawili ambapo Bunge la Japan pamoja na kuwa na kamati maalum
inayoshughulikia maswala ya Afrika, bado kuna haja kwa kamati hiyo
kufanya kazi kwa ukaribu na Bunge la Tanzania kwa lengo la kuangalia
maeneo muhimu ambayo Japan itaisaidia Tanzania.
Hata
hivyo Mhe. Yokomichi ameaidi kuishawishi Serikali yake ya Japan ili
iendelee kutenga fungu kubwa zaidi kwa lengo la kusaidia sekta
mbalimbali za maendeleo nchini Tanzania. Tarari Japan ni mchangiaji
Mkubwa katika sekta mbalimbali za maendelo kwa kiasi kikubwa.
Spika
wa Bunge Mhe. Anne Makinda na Ujumbe wa wabunge 5 kutoka Bunge la
Tanzania upo Japan kwa mwaliko maalum na Bunge la Japan kujadili na
kuimarisha ushirikiano baina ya Mabunge haya mawili, ambapo kabla ya
kuonana na Mwenyeji wake, Ujumbe huo wa Tanzania ulipata fursa ya
kutembelea maeneo mbali mbali ya utalii nchi Japan ikiwa ni pamoja na
eneo la Mji wa Natori lililokumbwa na mafuriko yaliotokea machi mwaka
jana na Mji wa Hiroshima uliosambaratishwa na Bomu la Atomic wakati wa
vita kuu ya dunia mwaka 1945. Spika na Ujumbe wake wanatarajia kurudi
nchini jumanne wiki hii.
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)