Mkataba wa ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilometa 22.1 kutoka Wete hadi Chakechake kisiwani Pemba wasainiwa - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Mkataba wa ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilometa 22.1 kutoka Wete hadi Chakechake kisiwani Pemba wasainiwa

Waziri wa Fedha Dkt William Mgimwa (kushoto) akibadilishana hati ya mkataba wa mkopo nafuu na Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Waarabu inayojishughulisha na Maendeleo ya Uchumi ya Afrika (BADEA) Bw. Abdelaziz Khelef (kulia)leo mjini Arusha wa mradi wa ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilometa 22.1 kutoka Wete hadi Chakechake kisiwani Pemba. Mradi huo utagharimu shilingi bilioni 15.
Waziri wa Fedha Dkt William Mgimwa (kushoto) akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari jana mjini Arusha mara baada ya kubadilishana hati ya mkataba wa mkopo nafuu na Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Waarabu inayojishughulisha na Maendeleo ya Uchumi ya Afrika (BADEA) Bw. Abdelaziz Khelef (kulia) wa mradi wa ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilometa 22.1 kutoka Wete hadi Chakechake kisiwani Pemba. Mradi huo utagharimu shilingi bilioni 15.
Waziri wa Fedha na Mipango Ofisi ya Rais Yusuf Omar Mzee (kushoto) akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari jana mjini Arusha juu ya umuhimu wa barabara mpya inayotarajiwa kujengwa kutoka ChakeChake hadi Wete kisiwani Pemba mara baada ya Tanzania na  Benki ya Waarabu inayojishughulisha na Maendeleo ya Uchumi ya Afrika (BADEA) kusaini mkataba wa mkopo wa masharti nafuu wa mradi wa ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilometa 22.1. Kulia ni Waziri wa Miundombinu ,Mawasiliano na Uchukuzi wa Serikali ya Zanzibar Hamad Masoud 
Naibu Waziri wa Fedha Saada Salum  (katikakati) akibadilishana mawazo na Msemaji wa Wizara ya Fedha Bi. Ingiahedi Mduma(kushoto) wakati wa mapumziko baada ya mikutano mbalimabli inayoendelea mjini Arusha ya Benki ya Maendeleo ya Afrika(AfDB). Kulia ni Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango ya Zanzibar Amina Khamis Shaaban.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages