Mh. Mohammed Raza
Na Khadija Khamis –Zahira Bilali –MAELEZO
Tume
ya Uchaguzi Zanzibar imemtangaza rasmi Mohamed Raza Hassanali
Mohamadali kuwa Mwakilishi halali wa Jimbo la Uzini kwa kushinda
asilimia 91.1 sawa na kura 5377.
Matokeo
hayo yametolewa na Afisa Msimamizi Uchaguzi wa Wilaya ya Kati Mussa
Ali Juma huko katika Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Kati Unguja.
Alisema kuwa zoezi la Uchaguzi mdogo wa Jimbo la Uzini ulikwenda
vizuri mpaka kufikia katua ya matokeo.Alisema kuwa Vyama
vilivyoshiriki katika zoezi hilo vilikuwa jumla ya vyama vitano
ndivyo vilivyoweza kusimamisha wagombea wake navyo ni AFP,CCM,CHADEMA
.CUF na TADEA .
Matokeo
ya uchaguzi huwo ulikuwa kama ifuatavyo kwa upande wa CCM mgombea wake
Mohamedraza alipata kura 5377, Rashid Yussuf Mchenga wa AFP alipata
kura 08 Khamis Khatib Vuai wa TADEA alipata kura 14 Salma Hussein
Zaral wa CUF amepata kura 223,na Ali Mbaruku Mshimba wa CHADEMA
alipata 281 .
Alieleza
kuwa jumla ya wananchi waliondikishwa katika uchaguzi huo ni 8743
waliyojitokeza kupiga kura 5931 kura halali 5903na kura zilizoharibika
28 .Nae Mgombea wa CCM aliebukia kuwa mshindi wa uchaguzi huo
aliishukuru Tume ya Uchaguzi kwa kuendesha zoezi hilo kwa ufanisi .
Pia
aliwahidi wananchi wake wa jimbo hilo kuwa atawatumikia bila ya
kujali ubaguzi na itikadi za kisiasa na kuwaletea maendeleo kwa
vitendo kama ilani ya chama chake inavyoeleza .Zoezi hilo la uchaguzi
limefanyika kutokana na kufariki kwa Mwakilishi wa Jimbo la Uzini
Marehemu Mussa Khamis Silima .
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)