Dina Marios:Women In Balance-Kitchen Party Gala ni 28 january 2012. - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Dina Marios:Women In Balance-Kitchen Party Gala ni 28 january 2012.

Mtayarishaji wa party hiyo na Mtangazaji wa Radio Clouds FM Dina (Kushoto)wakionesha DVD ya kitchen party gala iliyopita ambazo wanatarajia kuzitengeneza kwa wingi na zitaanza kupatikana mapema mwezi ujao,ambapo kila mwezi watakuwa wakirekodi,kwa wale watakaotaka kununua labda alipitwa zitakuwa zikipatikana.
--
Women In Balance-kitchen party Gala
Wasichana na wanawake wengi kwa sasa wanakabiliwa na changamoto nyingi sana ambazo zinapelekea kushindwa kusimama katika mahusiano yao.Teknolojia,mwamko wa elimu,wanawake kumiliki biashara binafsi,kazi,wazazi hawahusishwi ,kila mtu mjuaji ,kujisahau n.k
Matokeo yake talaka nyingi na mahusiano kuvunjika sasa tunataka kumkumbusha mwanamke wajibu wake na nafasi yake katika mahusiano.Ajitambue.
Msimu wa pili
Eneo hili limelenga kukuza ujuzi wa mwanamke katika Nyanja za kijamii zaidi.Kupitia eneo hili mwanamke atajifunza mambo mbalimbali kiasili na kisasa ambayo mwanamke anaengia au aliyeko au anaetegemea kuingia katika mahusiano na ndoa.Mambo kama malezi ya watoto ,nafasi yake katika jamii umuhimu kujiamini na mengineyo.
Wazo hili limekuja mara baada ya kuona kwamba ule muda wanawake wanaopata kuongea mambo haya kwenye kitchen party ni mchache na hautoshi kumfahamisha mwanamke mambo yote muhimu.Mambo ambayo ni lazima ayajue au hata kama anayajua kutokana na pilika pilika za maisha anajisahau.
Tukio hili kufanyika jumamosi hii ya tarehe 28 january 2012.Kuanzia saa nane mchana mpaka saa mbili usiku katika ukumbi wa Danken house uliopo mikocheni kwa warioba.
Watoa mada ni watu wenye uwezo katika swala zima la uelimishaji
Aunt sadaka;Ni mwana saikolojia aliyebobea katika maswala ya wanawake na watoto.Ana uwezo katika Nyanja hii ambao umetokana kielimi na uzoefu wa kukutana na kesi mbalimbali amabazo zinazo mguza mwanamke hivyo kuweza kuwa funzo kwa wengine.
Bi Chau ni mwanamke ambae mbali na kuwa katika fani ya sanaa kwa muda mrefu wamekua wakito amafunzokwa wanawake tokea muda mrefu.Mafunzo ya mahusiano,ndoa na familia kwa ujumla.
Mama Victor;Ni mtumishi wa Mungu katika dini ya kikristo ambae anaelimisha wanawake kwa mafunzo ya kidini.Anafundisha mwanamke kujitambua vile mungu amempa uwezo wa kuitumikia jamii yake kama mlezi na kiongozi.
Kwa ufupi hawa ndio wakufunzi katika tukio letu hili la women in Balance jumamosi hii katika msimu wa pili.
Burudani itatolewa na Nyota Waziri.
Huu ni mkakati wa mwaka mzima huu 2012 na tutakutana kila mwezi mpaka mwezi march ambapo ratiba itabadilika na wanaume kuhusishwa.
WADHAMINI WETU WA SIKU HII NI
BAILEYS (kinywaji),MGen insuarance,cocacola,cooperate image na clouds fm.
IMETOLEWA NA MRATIBU WA WOMEN IN BALANCE
DINA MARIOS.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages