Standard Chartered wachangia 1.1% ya GDP ya Tanzania - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

demo-image

Standard Chartered wachangia 1.1% ya GDP ya Tanzania

MEZA+KUU
 Mgeni rasmi Katibu Mkuu Wizara Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof Elisante Ole Gabriel (katikati) akibadilishana mawazo na Mkuu wa Makampuni na Taasisi za Fedha wa benki ya Standard Chartered, Jaffer Machano (kulia) mara baada ya kuwasili kwenye hafla ya uzinduzi wa ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii nchini iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha ni Kutoka kushoto ni Mwandishi wa ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii, Rene Kim, Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa benki ya Standard Chartered nchini Tanzania, Ruth Zaipuna, Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dk. Bernard Kibesse pamoja na Mmoja wa wajumbewa bodi ya benki ya Standard Chartered nchini, Harish Bhatt (wa pili kulia).
NAIBU+GAVANA
 Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dk. Bernard Kibesse (kushoto) akibadilishana mawazo na Mgeni rasmi Katibu Mkuu Wizara Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof Elisante Ole Gabriel (katikati) pamoja na Mmoja wa wajumbewa bodi ya benki ya Standard Chartered nchini, Harish Bhatt (kulia) wakati wa hafla ya uzinduzi wa ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii nchini iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
PS+CHEKA
 Mgeni rasmi Katibu Mkuu Wizara Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof Elisante Ole Gabriel akifurahi jambo na na Mmoja wa wajumbewa bodi ya benki ya Standard Chartered nchini, Harish Bhatt wakati wa hafla ya uzinduzi wa ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii nchini iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
PS+na+JUANITA
 Mgeni rasmi Katibu Mkuu Wizara Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof Elisante Ole Gabriel akizungumza jambo na Mkuu wa Mahusiano na Masoko wa Benki ya Standard Chartered, Juanita Mramba wakati wa hafla ya uzinduzi wa ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii nchini iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
HIGH+TABLE
 Meza kuu kutoka kushoto ni Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dk. Bernard Kibesse, mgeni rasmi Katibu Mkuu Wizara Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof Elisante Ole Gabriel, Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa benki ya Standard Chartered nchini Tanzania, Ruth Zaipuna pamoja na Mwandishi wa ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii nchini, Rene Kim.
PS+SPEECH+1
 Mgeni rasmi Katibu Mkuu Wizara Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof Elisante Ole Gabriel akizungumza na wafanyakazi wa benki ya Standard Chartered na wageni waalikwa (hawapo pichani) wakati wa hafla ya uzinduzi wa ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii nchini iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
GAVANA+SPEECH
  Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dk. Bernard Kibesse akizungumza wakati wa uzinduzi wa ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii nchini iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
ACTING+CEO+SPEECH
 Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa benki ya Standard Chartered nchini Tanzania, Ruth Zaipuna akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Katibu Mkuu Wizara Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof Elisante Ole Gabriel (kushoto) kuzindua rasmi ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii nchini iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
RENE+KIM
 Mwandishi wa ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii nchini, Rene Kim akifanya mchanganuo wa ripoti hiyo kabla ya kuzinduliwa kwa ripoti hiyo kwenye hafla iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
JAFFER
 Mmoja wa wajumbewa bodi ya benki ya Standard Chartered nchini, Harish Bhatt (kushoto) pamoja na Mkuu wa Makampuni na Taasisi za Fedha wa benki ya Standard Chartered, Jaffer Machano wakati wa hafla ya uzinduzi wa ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii nchini iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
ZINDUA+1
ZINDUA+2
 Katibu Mkuu Wizara Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof Elisante Ole Gabriel (wa pili kulia), Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dk. Bernard Kibesse pamoja na Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa benki ya Standard Chartered nchini Tanzania, Ruth Zaipuna wakizindua rasmi ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii nchini iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Mkuu wa Makampuni na Taasisi za Fedha wa benki ya Standard Chartered, Jaffer Machano (kulia) na kushoto ni Mmoja wa wajumbewa bodi ya benki ya Standard Chartered nchini, Harish Bhatt.
ZINDUA+3
 Mgeni rasmi Katibu Mkuu Wizara Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof Elisante Ole Gabriel (wa pili kulia), Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dk. Bernard Kibesse(wa pili kushoto), Mmoja wa wajumbewa bodi ya benki ya Standard Chartered nchini, Harish Bhatt (kushoto),  Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa benki ya Standard Chartered nchini Tanzania, Ruth Zaipuna (wa tatu kulia) pamoja na Mkuu wa Makampuni na Taasisi za Fedha wa benki ya Standard Chartered, Jaffer Machano (kulia) wakipiga makofi baada ya kuzinduliwa rasmi ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii nchini iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
STAFF+1
STD+STAFF+1
 Baadhi ya wafanyakazi wa wa benki ya Standard Chartered waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki hiyo kwa uchumi na jamii nchini, iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
WADAU+1
WADAU+2
WADAU+3
WADAU+4
WADAU+5
CROSS+SECTION
 Sehemu ya wateja wa benki ya Standard Chartered, wafanyakazi wa benki hiyo, wanahabari pamoja na wageni waalikwa waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki hiyo kwa uchumi na jamii nchini, iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
PS+AGA
 Mkuu wa Mahusiano na Masoko wa Benki ya Standard Chartered, Juanita Mramba (kushoto) akizungumza jambo na mgeni rasmi Katibu Mkuu Wizara Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof Elisante Ole Gabriel (kulia)alipokuwa akijiandaa kuondoka ukumbini hapo. Wengine ni Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dk. Bernard Kibesse(wa pili kulia)pamoja na Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa benki ya Standard Chartered nchini Tanzania, Ruth Zaipuna.
GROUP+PHOTO
Mgeni rasmi Katibu Mkuu Wizara Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof Elisante Ole Gabriel (wa tatu kulia) katika picha ya pamoja na meza kuu mara baada ya kuzindua ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki ya Standard Chartered kwa uchumi na jamii nchini iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.













Standard Chartered wachangia 1.1% ya GDP ya Tanzania

Na Mwandishi wetu

BENKI ya Standard Chartered imechangia asilimia 1.1 ya pato la taifa (GDP) sawa na kuwezesha huduma na bidhaa zenye thamani ya dola milioni 579.

Taarifa hiyo imetolewa wakati wa uzinduzi wa ripoti ya athari chanya ya mchango wa benki hiyo kwa uchumi na jamii nchini iliyofanyika katika hoteli ya Serena.

Alisema mchango wake pamoja na kusaidia upatikanaji wa kazi, biashara na ukuaji wa uchumi, imekuwa ikichangia maendeleo ya ukuaji wa sekta ya fedha katika miundombinu na utaalamu.

Katika uzinduzi huo uliofanywa na Katibu Mkuu Wizara Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof Elisante Ole Gabriel, Benki hiyo imesema kwamba imewezesha nafasi za kazi za moja kwa moja na za msaada zipatazo 220,000 ikiwa ni sawa na asilimia moja ya watanzania wote walioajiriwa.

Kuhusiana na mchango wake katika uchumi wa Tanzania, ripoti inaonesha kwamba Standard Chartered Bank inahusika na ukuaji wa sekta ya biashara kwa asilimia 3.5 na katika viwanda ikiwa ni asilimia 3.7.

Pamoja na kutoa takwimu za mchango wake katika uchumi wa Tanzania, pia ripoti hiyo imeonesha namna bora ambapo benki inaweza kukuza mchango wake katika uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla.

Benki imeshauri kufanya mambo kadhaa ikiwamo kuongeza shughuli zake za kuchochea ukuaji wa biashara kwa nchi za Afrika Mashariki na kujiimarisha katika soko hilo.

Kuelekeza nguvu zake katika sekta ya uzalishaji bidhaa kwa kusaidia kampuni za ndani kusonga mbele katika uzalishaji wa bidhaa na hivyo kuongeza kasi ya ukuaji wa kiuchumi.

Aidha imeelezwa benki hiyo ina fursa bado za kusaidia watu maskini, ambao ni lazima kuwasaidia kukua kimapato na hivyo kukuza uchumi. Kwa kukua kwa kipato chao Benki itaongeza idadi ya watu wanaotakiwa kuwa wateja wao hapo baadae.

Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa benki hiyo nchini Tanzania, Ruth Zaipuna, amesema kwamba ripoti hiyo imeonesha mchango wa benki ukuaji wa kiuchumi na hasa sekta binafsi ambayo ndio inatoa wateja.

Alisema benki hiyo itaendelea kufanya juhudi za kuimarisha ushirikiano wake na mataifa ya Afrika Mashariki kupitia bidhaa zake mbalimbali.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Pages