Shindano la MO Margarine Star kutoa zawadi ya mil 4.2 kwa wanafunzi 10 nchini - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Shindano la MO Margarine Star kutoa zawadi ya mil 4.2 kwa wanafunzi 10 nchini

Kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MeTL Group) imeandaa shindano la kuimba wimbo wa MO Margarine kwa wanafunzi wa elimu ya msingi na sekondali, linalokwenda kwa jina la ‘MO Margarine Star’.
Akizungumza kuhusu shindano hilo, Mkurugenzi wa Masoko wa MeTL Group, Fatema Dewji ametoa masharti ya shindano hilo, kwamba kabla ya mwanafunzi kushiriki shindano hilo anatakiwa apate ridhaa kutoka kwa wazazi ama walezi wake.

Ameeleza kuwa, ili kushiriki shindano hilo, mwanafunzi anatakiwa ajirekodi video akiimba wimbo huo, na kuposti katika akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Instagram au Facebook kisha kuishirikisha akaunti ya METL inayopatikana na kuweka hashtag ya #MoMargarineStar.
Dewji alisema zawadi kwa washindi ni Sh. 700,000 kwa mshindi wa kwanza, Sh. 600,000 kwa mshindi wa pili, Sh. 500,000 kwa mshindi wa tatu na kuanzia mshindi wa nne hadi 10 watapewa Sh. 400,000 kwa kila mmoja.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages