SIKU YA TATU YA KUELEKEA KILELE CHA UHURU KATIKA MLIMA KILIMANJARO KWA WAZALENDO 47 KWA AJILI YA MAADHIMISHO YA MIAKA 56 YA UHURU PAMOJA NA KUTANGAZA UTALII WA NDANI NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA. - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

demo-image

SIKU YA TATU YA KUELEKEA KILELE CHA UHURU KATIKA MLIMA KILIMANJARO KWA WAZALENDO 47 KWA AJILI YA MAADHIMISHO YA MIAKA 56 YA UHURU PAMOJA NA KUTANGAZA UTALII WA NDANI NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA.

E79A0259
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Mstaafu,Jenerali,George Waitara akiwa katika maandalizi ya kuianza siku ya tatu ya Wazalendo 47 kuelekea katika kilele cha Uhuru ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 56 ya Uhuru .
E79A0266
Baada ya kupumzika kwa muda katikia kituo cha Horombo Wazalendo kutoka Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) ,Waandishi wa Habari,Marafiki wa China na Tanzania pamoja na Watumishi wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) walianza safari ya kuelekea kituo cha mwisho cha Kibo kabla ya kuelekea kilele cha Uhuru.
E79A0278
E79A0285
E79A0290
Safari ilianza kwa Slogan ile ile ya "Mdogo Mdogo"
E79A0300
Baadae Safari ikaingia kwenye barabara yenye mawe hivyo utembeaji katika eneo hili ulihitaji uangalifu wa hali ya juu.
E79A0319
Wengine walitengeneza Tabasamu kuonesha safari itamalizika kwa salama.
E79A0328
E79A0330
E79A0334
Safari iliendelea na kila mmoja alipambana na hali yake.
E79A0339
Hatimaye Wazalendo wakaiacha misitu mifupi bna kuingia katika kituo cha mwisho kabisa yanapotiririka maji.
E79A0350
E79A0384
Hapa Wanapaita "Last Woter Point"
E79A0397
Wazalendo wakafika Last Woter Point na kupata mapumziko ya muda mfupi wakiongozwa na Mwogoza watalii Mkuu,Faustine Chombo kutoka kampuni ya Utalii ya Zara.
E79A0414
Safari ikaingia eneo la mchanga maarufu kama Saddle.hali ya hewa ya eneo hili imekuwa ya kubadiliko kila baada ya dakika chache
E79A0425
Unaweza tembea usimuone mwenzako yupo wapi kutokana na hali ya Ukungu na wakati mwingine mvua ambayo imekuwa ikinyeskatika eneo hilo.
E79A0434
Safari ya muda mrefu ikaelekea katika kituo cha mapumziko cha Kibo Hut.
E79A0435
Wazalendo Wakaingia Kibo Hut kwa ajili ya maandalizi ya kuelekea kilele cha Uhuru,usiku wa saa tano.
E79A0447
Baadhi ya Wazalendo wakiongozwa na Meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za taifa (TANAPA) Pascal Shelutete wakapata Taswira katika kibao cha Kibo Hut ikiwa ni urefu wa Mita 4720 kutoka usawa wa bahari zikisalia mita 1175 kufika kilele cha Uhuru.
E79A0445
Wazalendo wakipata kumbukumbu katika kituo cha Kibo Hut .

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii ,Kanda ya Kaskazini aliyekuwa katika safari hiyo.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Pages