SAFARI YA WAZALENDO 47 ILIVYOINGIA SIKU YA PILI WAKATI WAKIELEKEA KILELE CHA UHURU,KATIKA MLIMA KILIMANJARO - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

demo-image

SAFARI YA WAZALENDO 47 ILIVYOINGIA SIKU YA PILI WAKATI WAKIELEKEA KILELE CHA UHURU,KATIKA MLIMA KILIMANJARO

E79A0013
Baada ya kupumzika katika kituo cha Mandara katika siku ya kwanza ,Mkuu wa Majeshi Mstaafu,Jenerali George Waitara aliongoza Wazalendo 47 kutoka jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ),Wanahabari,Marafiki wa China na Tanzania pamoja na watumishi kutoka Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) katika siku ya pili ya kuelekea kilele cha Uhuru kwa ajili ya maadhimisho ya miaka 56 ya uhuru wa Tanzania.
E79A0015
Miongoni mwao alikuwepo ,Balozi Mstaafu na Mwenyekiti Mstaafu wa Bodi ya Utalii ,Tanzania ,Charles Sanga.
E79A0018
E79A0023
E79A0025
Safari ya kuelekea kituo cha pili cha mapumziko cha Horombo ili chagizwa na nyimbo mbalimbali ambazo ziliongeza morali kwa wapandaji.
E79A0027
Makao makuu ya Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) yaliwakilishwa vyema na Meneja wake wa Mawasiliano ,Pascal Shelutete .
E79A0031
Mwanahabri Vicky Kimaro aliwakilisha pia Magazeti ya serikali ya HABARI LEO.
E79A0036
Mwanahabari George Mbara alikiwalisha vyema kituo cha luniknga cha ITV.
E79A0043
Mwanahabari Jamila Omar yeye alifanya uwakilishi wa kituo cha Luninga cha Channel ten.
E79A0040
Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) liliwakilishwa na Bertha Mwambela 
E79A0054
Na Safari iliendelea ikiongozwa na Slogan ya "Mdogo Mdogo"
E79A0067
Mapumziko yalikuwepo mara baada ya kutembea sehemu yenye umbali mrefu.
E79A0082
Wengine walitumia mapumziko hayo kwa ajili ya kupata picha za kumbukumbu ya pamoja.
E79A0088
Na baadae Safari iliendelea.
E79A0117
Hali ya hewa katika Hifadhi ya taifa ya Mlima Kilimanjaro haitabiliki ghafla linaweza onekana jua na muda mchache tu mvua ikanyesha ,hivyo wapandaji hua wamejiandaa na aina yoyote ile ya hali kama inavyoonekana hapa wakiwa katika mavazi rasmi ya kuzuia mvua pindi walipowasili eneo la Nusu njia kwa ajili ya kupata chakula.
IMG_2933
IMG_2939
Wazalendo wakatumia mapumziko ya Nusu njia kupata chakula cha mchana.
IMG_2951
Safari ikaendelea kwa kupita katika mito mbalimbali ambayo imekuwa ikitiririsha maji kwa wingi.
IMG_2961
Wazalendo walipita katika madaraja mbalimbali wakati wa upandaji wa mlima huo.
IMG_2976
Wenye kuhitaji msaada walipata kwa wakati.
IMG_2975
IMG_2984
Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro (KINAPA) Betrita Loibook alihakikisha anaongozana na Wazalendo hao katika safari ya kuelekea kilele cha Uhuru akiwa ndiye mwenyeji wa ugeni huo.
IMG_2969
Hatimaye safari iliyoanza saa 2:30 za asubuhi katika kituo cha mapumziko cha Mandara ikahitimishwa majira ya saa 11:00 za jioni katika kituo cha mapumziko cha Horombo kwa ajili ya kujiandaa na safari ya kuelekea kituo cha Kibo kabla ya kuelekea kilele cha Uhuru.

Na Dixon Busagaga wa Globu kanda ya Kaskazini aliyekuwa katika msafara wa Wazalendo hao.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Pages